Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mastaa tisa wampasua kichwa Ibenge

Muktasari:

  • Juzi kocha wa timu ya Taifa Taifa Stars, Miguel Gamondi aliita kikosi kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya AFCON 2027 huku Azam ikiwa na wachezaji wengi zaidi kuliko timu nyingine zote, baada ya mastaa tisa wa timu hiyo kuitwa kati ya wachezaji 42.

KOCHA wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema anafurahia kuona wachezaji wake tisa wameitwa kwenye kikosi cha Taifa Stars, lakini amekiri hatua hiyo imemuweka kwenye changamoto kubwa katika maandalizi ya kikosi chake.

Juzi kocha wa timu ya Taifa Taifa Stars, Miguel Gamondi aliita kikosi kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya AFCON 2027 huku Azam ikiwa na wachezaji wengi zaidi kuliko timu nyingine zote, baada ya mastaa tisa wa timu hiyo kuitwa kati ya wachezaji 42.

Akizungumza na Mwanaspoti Ibenge alisema wachezaji hao ni sehemu muhimu ya mipango yake, hivyo kuondoka kwao kwenda kwenye majukumu ya Taifa kunapunguza muda aliokuwa ameupanga kuutumia wakati wa mapumziko ya mechi za kimataifa za FIFA katika kujenga muunganiko wa kikosi chake.

Mastaa wa Azam walioitwa ni Zuberi Foba, Aishi Manula, Lameck Lawi, Twalib Nuru, Pascal Msindo, Himid Mao, Feisal Salum, Abdulkarim Kiswanya na Abdul Suleiman.

Alisema kuwa, kipindi hicho kilikuwa muhimu kwake baada ya muda wa maandalizi ya msimu mpya kutokuwa wa kutosha katika kambi ya maandalizi ya msimu ‘pre-season’.

Alisema sasa atalazimika kutumia mbinu nyingine kuhakikisha anawafanyia maboresho wachezaji watakaobaki kambini, huku akisubiri kurejea kwa wale watakaokuwa kwenye majukumu ya Taifa.

“Ninafurahia kuona wachezaji wangu tisa wameitwa Taifa Stars kwa sababu hii ni heshima kwao na kwa klabu. Lakini kwa upande mwingine, hii ni changamoto kwetu kwa sababu tulitaka kutumia kipindi hiki cha mapumziko kujenga muunganiko wa timu,” alisema Ibenge.

Kocha huyo aliongeza kuwa wachezaji hao tisa ni muhimu katika mfumo anaotaka kuutumia msimu huu, hivyo kutokuwepo kwao kunamlazimisha kutafuta njia mpya za kuhakikisha muda uliopo hautapotea.


Kikosi kamili:

MAKIPA

1. Zuberi Foba — Azam FC

2. Aishi Manula — Azam FC

3. Yona Amos — Singida Black Stars

4. Metacha Mnata — Singida Black Stars

5. Hussein Masalanga — Young Africans


MABEKI

6. Ibrahim Bacca — Young Africans

7. Bakari Mwamnyeto — Young Africans

8. Lameck Lawi — Azam FC

9. Twalib Nuru — Azam FC

10. Vedastus Masinde — Simba SC

11. Mohammed Mussa — Young Africans

12. Danillo Maino — FK Panevezys, Lithuania

13. Haji Mnoga — Patro Eisden, Ubelgiji

14. Bakari Msimu — Simba SC

15. Nickson Kibabage — Simba SC

16. Mohammed Hussein — Young Africans

17. Anthony Mlugo — Simba SC

18. Pascal Msindo — Azam FC

19. Nathaniel Chilambo — Simba SC


VIUNGO

20. Novatus Miroshi — Göztepe, Uturuki

21. Himid Mao — Azam FC

22. Adolph Mtasigwa — Kaizer Chiefs, Afrika Kusini

23. Yusuf Kagoma — Simba SC

24. Mohamed Sagaf — Eastbourne Borough, Uingereza

25. Alphonse Mabula — JS Kabylie, Algeria

26. Charles Mmombwa — Zabbar, Malta

27. Mudathir Yahya — Young Africans

28. Feisal Salum — Azam FC

29. Sheikhan Khamis — Singida Black Stars

30. Morice Abraham — Simba SC

31. Abdulkarim Kiswanya — Azam FC


WASHAMBULIAJI

32. Tarryn Allarakhia — Boreham Wood, Uingereza

33. Simon Msuva — Newroz, Iraq

34. Bernard Kamungo — FC Dallas, Marekani

35. Kelvin John — Aalborg, Denmark

36. Kibu Denis — Al Nasr, Libya

37. Abdul Suleiman — Azam FC

38. Sabri Kondo — Häcken, Sweden

39. Cyprian Kachwele — HFX Wanderers, Canada

40. Said Khamis — Hajafungamana na timu

41. Selemani Mwalimu — Young Africans

42. Paul Peter — JKT Tanzania