Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Masau ampiga dongo Morrison

ILE staili ya ushangiliaji ya nyota wa Simba, Benard Morrison kwenye mchezo wa juzi dhidi ya Al Hilal ya Sudan imezua mijadala huko mitandaoni na mmoja wa wadau ambaye hajapitwa na hilo ni Masau Bwire.

Kama ambavyo mnamfahamu Masau Bwire ametumia ukurasa wake wa mtandao wa Kijamii wa Instagram kusema kile aombacho mtu hupewa. Hakuishia hapo, maneno yake yalisomeka, “Aombacho mtu hupewa. Huyu bingwa naona anaomba kutune kama mpira wa miguu. Kwa kuwa Mungu si Athumani, siku ombi lake likijibiwa, asipige kelele.”

Masau akatoa nafasi kwa wafuasi wake kwa kuwauliza wanasemaje juu ya tukio lile, wapo ambao walikuwa wakimuunga mkono kutona na alichokiandika lakini asilimia kubwa ya mashabiki wa Simba waliona ni kama msemaji huyo wa Ruvu Shooting anawaonea wivu tu.

Hivi karibuni kulikuwa na maneno kuwa Mghana huyo alikuwa akiumwa kitu ambacho alikanusha kwamba hakuwa mgonjwa wa kile ambacho walikuwa wakikisema ndio maana alishangilia vile.