Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kipanga ipo tayari kwa msimu mpya

KIPANGA Pict

Muktasari:

  • Amesema wanatarajia msimu huu utakuwa na ushindani mkubwa kuliko uliopita na kuvutia kwa sababu timu nyingi zimeboresha vikosi vyao , lakini hilo haliwatishi kwani nao wamejipanga vizuri.

IKIWA zimebaki siku chache kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Zanzibar, Kocha wa Kipanga, Khamis Hassan Makame 'Kocha Meki' amesema wapo tayari  kwa ajili ya mapambano..

Amesema mikakati yao ni kukamilisha malengo yao ambayo wameshindwa kuyatimiza msimu uliopita ndiyo maana wamefanyia maboresho kikosi chao kwa asilimia kubwa.

Ligi hiyo inatarajiwa kuanza Agosti 29, 2026 huku mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya KVZ na KMKM ukichezwa  Agosti 23.

Katika kufikia hayo, Kocha Meki amesema wanaendelea na mazoezi katika Uwanja wa Mtoni, hadi kufikia sasa timu ipo vizuri na kuimarika na inaendelea vizuri huku timu ikiimarika kila siku.

"Wachezaji wetu wengi wamesharipoti kambini ingawa kuna baadhi yao wachache bado hawajaripoti lakini nategemea kuanzia wiki ijayo wote watakuwa wameshafika na kujiunga na wenzao," amesema

Amesema wanatarajia msimu huu utakuwa na ushindani mkubwa kuliko uliopita na kuvutia kwa sababu timu nyingi zimeboresha vikosi vyao , lakini hilo haliwatishi kwani nao wamejipanga vizuri.