Dili iliyokufa - 44
ILIPOISHIA
Hapo ndipo nilipokumbuka. Wakati ule nilipokuwa nakwenda kwake kufuatia dawa ya mume wangu akanichukua hadi mahali hapo ambapo alikwenda kuniingiliakimwili akajidaiananifanyia dawa, kumbe alikuwa akinizuga mimi. Na kutoka siku ile sikutamani tenakurudi kwa mume wangu.
Sasa kilichomshinda mganga huyokukieleza wazi ni kuniambiakwamba mahali hapo ni pale tulipokwenda akaniingiliakimwili.
“Nimeshapakumbuka”nikamwambia.
SASA ENDELEA...
ILIPOISHIA
“Siku zako za kuishi zinaisha leo. Mimi ni Kashkash,jini mnywa damu za watu kila mwaka mara tatu…mimi ndiye niliyekuchagua uolewe na kiti wangu ili muda ukifika ninywe damu yako. Sasa muda huo umeshafika, tulia nilekaramu yangu…!”
Mikono yake ikanivamia ghafla. Nilipiga ukulele mmoja tu kisha sauti yangu ikapotea. Niliendelea kupiga kelele lakini sauti ilikuwa haisikiki. Nilikuwa kama ninayepiga kelele kimoyomoyo au kwenye ndoto.
SASA ENDELEA...
Nikaona meno ya yule mganga yakisogea kwenye shingo yangu na kuning’ata kwenye mshipa wa shingo.
Nilisikia maumivu makali kisha damu ikaanza kunitoka. Nikaendelea kupiga kelele zisizosikika.
“Jamani… nakufa…jamani nakufa…!”
Mganga huyo aliyekuwa amebadilika na kuwa jini alianza kunifyonza damu kwenye shingo.
Nguvu zilikuwa zikiniishia na sikuweza hata kujisogeza. Nilichoweza kufanya ni kuendelea kupiga kelele za kimoyomoyo.
“Jamani nakufa…jamani nakufa…!”
Ghafla nikasikia mlio wa risasi ya bunduki huko nje halafu nikasikia mlio wa mabuti yakienda huku na huko.
Nikasikia risasi nyingine ikipiga ndani ya kile chumba. Jinsi ule mlio ulivyovuma masikioni mwangu nilihisi kama ilipigwa kwa karibu na nilipigwa mimi. Yule mganga aliniachia akageuka nyuma.
Nilivyoachiwa nilijiona ninaanguka chini. Kabla sijafika chini nikadakwa. Sikuweza kujua nilidakwa na nani.
“Wewe ni nani na unamfanya nini huyu mwanamke?” nikasikia sauti ya amri ikiuliza.
“Mama inuka!” nikasikia sauti nyingine ikiniambia huku nikiwa nimeshikwa mkono.
Nikaunuka.
Sasa nikaweza kuangaza macho yangu vizuri. Niliona wale watu walikuwa polisi. Walikuwa polisi watatu mmoja wao akiwa mwanamke. Wote walishika bunduki.
“Wewe nani?” ile sauti iliyokuwa ikimuuliza yule mganga ilirudia kumuuliza.
“Mimi…mimi…unaniuliza mimi nani katika nyumba yangu, kwani wewe nani?” Mganga akaunguruma.
“Sisi ni polisi” sauti ikamjibu.
“Mnataka nini?”
“Wewe ndiye mganga tapeli unayetorosha wake za watu halafu…”
“Hebu mtoe nje tumuone vizuri…”
“Mbona kama ana meno marefu na macho yake hayana mboni kisha anatoka damu mdomoni….?” Ilikuwa sauti ya yule polisi mwanamke.
Yule mganga alivutwa na kutolewa nje kama jambazi. Tulipotoka huko nje niliuona uso wake ulikuwa wa kawaida. Haukuwa na macho meupe wala meno marefu.
Sikujua alibadilikaje ghafla.
“Mnasemaje… mnaseje?” mganga huyo akauliza kama vile alikuwa hajui lililotokea. Sauti yake sasa ilikuwa ya kawaida. Haikuwa ile ya kukoroma.
Joho lake lilikuwa limejaa matone ya damu yangu na mimi damu ilikuwa ikinitiririka kwenye shingo.
Kulikuwa na polisi wengine wawili waliokuwa huko nje pamoja na mume wangu. Walikuwa wamewashikilia wale wake wawili wa mganga, mke mkubwa na mke mdogo ambaye sikuweza kujua alifikajepale kwa maana hakuwepo kwenye msafara wetu.
Polisi waliiona ile damu iliyokuwa ikivuja kwenye shingo yangu.
“Na hii damu inatoka wapi?” Yule polisi mwanamke akauliza kwa mshangao huku akiitazama damu hiyo kwenye shingo yangu na kwenye lile joho la mganga.
“Alikuwa amening’ata na kuniifyonza damu” nikawambia polisi.
Nilivyotamka hivyo yule polisi mwanamke alimpiga kibao yule mganga. Kilikuwa kibao kikali kwani alipopigwa aliguna akajishika shavu.
“Unamfyonza damu binaadamu mwenzako kwa maana gani?” akamuuliza.
Mganga akanyamaza kimya. Sasa alikuwa amenywea. Huwezikuamini kwamba ndiye yule aliyekuwa akiniambia “Siku zako za kuishi zinaisha leo…mimi ni Kashkash…”
“Alikuwa anataka kuniua. Aliniambia siku zangu za kuishi zinaisha leo…” nikaendelea kuwambia wale polisi huku nikijipapasa ile sehemu niliyokuwa ninatoka damu.
“Siku zake yeye za kutapeli watu na kutorosha wake za watu ili awaue ndio zinaisha leo. Mshenzi mkubwa!” Polisi mmoja akamwambia.
“Na hawa wake zake ndio vibaraka wake. Wanajua kila kitu. Wote tutawafungulia mashitaka”
“Mimi simo. Mwenyewe nilikuwa nimelalanyumbani, sijisikii vizuri” yule mke mdogo akajitetea.
“Nyote nyinyi mnahusika” Polisi mwanamke akawambia.
“Sogeza gari” Polisi mwingine akasema.
Nikaona gari la polisi linakuja mbele ya ile nyumba.
Yule mganga pamoja na wake zake wawili wakapakiwa kwenye gari hilo.
“Hebu tuingie humu ndani tufanye upekuzi” Polisi mmoja akasema.
Yeye na polisi wenzake wawili wakaingia ndani ya ile nyumba.
Baada ya muda wa kama robo saa hivi walitoka wakiwa wameshika sanduku la mbao. Wakaliweka chini.
“Huyu mtu alikuwa mnyama kweli” Mmoja wa polisi hao akasema kisha akaongeza.
“Humu ndani ya sanduku mna vichwa vitayu vya binaadamu”
Alilifungua lile sanduku. Tulipotupa macho yetu tukaviona vichwa hivyo vilivyokuwa vimekaushwa. Kichwa kimoja kilinifanya nigutuke.
Kilikuwa na sura ya mwanamke ambaye nilikuwa nikimuona nyumbani kwa yulemganga siku za mwanzo mwanzo halafu baadaye nikawa simuoni tena. Lakini katika akili yangu nilikuwa namhisi kama alikuwa mmoja wa wake zake, yaani mke wake wa tatu kabla yangu.
Nikakisia kwamba mwanamke huyo atakuwa amefyonzwa damu na kuchinjwa na kisha kichwa chake kuhifadhiwa katika lile sanduku. Kwa hiyo hata vile vichwa vingine vilikuwa vya watu waliofyonzwa damu na kuchinjwa.
Pale niligunudua kwamba yule mganga hakuniroga nikae kwake kwa kunipenda bali alitaka anitoe mhanga kwa majini wake kama alivyomtoa mhanga yule mwanamke wake mwingine.
Loh! Kama si juhudi ya wifi yangu kuja kwa mganga huyu na kufanyiwa ule uganga uliorudisha akili yangu, siku ile ningefyonzwa damu na kuchinjwa bila mume wangu kujua.
Nikatikisa kichwa changu kusikitika. Kumbe hawa waganga wana mengi, tunawapenda sana lakini wana hila. Wewe unakwenda akushughulikie tatizo lako kumbe yeye ana lake jambo!
Wale polisi wengine walipoviona vichwa hivyo walishituka.
“Hivi vichwa ni vya nani?” Mmoja wa wale polisi aliyetoka nalile sanduku akamuuliza mganga huyo aliyekuwa kwenye gari.
Mganga akavitazama kisha akabetua mabega.
“Sijui ni vichwa vya nani” akasema.
Yule polisi alimsogelea na kumtandika bonge la bao!
“Unasema hujui ni vichwa vya nani? Wewe si ndiye uliyewachinja hawa! Miili yao iko wapi?”
Mganga akanyamaza kimya. Akatandikwa bao jingine.
“Usiposema leo tunakuua hapa hapa mpumbavu wewe!. Tunajua hawa watu umewaua wewe, miili yao iko wapi?”
Mganga alipoanza kujitafuna tafuna, polisi huyo alimkwida kwa hasira akamuinua juu na kumshusha kwenye gari.
Kile kitendo cha kukwidwa ghfla na kushushwa kwenye gari kama mzigo kilimfanya mganga agwae na kuhisi kitakachofuata baada ya hapo ni kipigo mwizi!
“Iko wapi miili yao?”Polisi huyo akamuuliza kwa sauti ya ukali akiwa bado amemshikilia kwenye ukosi.
“Niliizika…” Mganga akasema kwa sauti iliypfifia.
“Umeizika wapi, hebu tuoneshe?”
Mganga huyo alinyoosha mkono kuonesha kwenye ule mzimu wake.
“Wapi…tuoneshe…!” Polisi huyo akaendelea kumuuliza.
“Kwenye ule mzimu”
“Mzimu uko wapi?”
“Huu hapa”
Mganga aliuonesha ule mzimu wake.
“Hebu njoo unioneshe” Polisi aliendelea kumkazania.
Akiwa bado amekwidwa, mganga alimpeleka polisi huyo kwenye ule mzimu.
“Nimewazika humu ndani” akamwambia.
“Twende humo ndani”
Wakaingia. Mimi na mume wangu pamoja na polisi wawili tukawafuata.
“Hebu mulika tochi” Polisi aliyemshikilia mganga akamwambia polisi aliyekuwa na tochi ambaye alikuwa nyuma yake.
Polisi huyo akamulika tochi mbele na kukiondoa kiza kilichokuwa kimetanda.
Walipoingia katika lile eneo, mganga aliwaonesha kaburi lililokuwa chini ya kile kichanja chake ambacho siku ile alinipandisha hapo na kunibaka.
Polisi aliyekuwa amemshika ukosi mganga huyo alimuachia na kumuuliza.
“Hebu tuoneshe vizuri umewazika wapi?”
“Nimewazika hapa”
Mganga alionesha chini ya kile kichanja.
“Umewazika hapa?”
“Ndiyo”
“Nani ni kwanini umewazika hapa?’
“Ndiyo mizimu ilivyotaka”
“Sasa ondoa hicho kichanja tulione hilo kaburi”
Mganga hakukataa. Akaanza kukisogeza kile kichanja.
“Na hicho kichanja ni cha nini?”
“Nicha wenyewe” Mganga alijibu huku akiendelea kuburutana na kichanja hicho.
“Wenyewe kina nani?”
“Wenye huu mzimu”
“Maneno ya kijinga sana. Hebu kiondoe haraka.
Wakati mganga anakiburuta kichanja hicho kukiweka pembeni, polisi huyo alikisukuma kwa nguvu na kukipindua. Polisi mwingine akasaidia kukisukuma hadi pembeni mwa mzimu huo.
Mchanga wa mahali kilipoondoka kichanja hicho ulikuwa umetitia.
“Hapa ndipo ulipoizika hiyo miili?” Polisi akamuuliza mganga huyo.