Riyama, mumewe kumbe hivi!
Muktasari:
- Riyama na Mysterio walifunga ndoa Juni 16, 2016 na Juni 2026 wakatimiza miaka 10 ya ndoa yao, licha ya mara kadhaa kuibuka kwa taarifa zinazowatenganisha.
STAA wa filamu nchini, Riyama Ally, ameibuka na kauli kuhusu taarifa za kutengana na mume wake, Leo Mysterio, baada ya Mwanaspoti kuwanasa hivi karibuni wakiwa pamoja.
Riyama na Mysterio walifunga ndoa Juni 16, 2016 na Juni 2026 wakatimiza miaka 10 ya ndoa yao, licha ya mara kadhaa kuibuka kwa taarifa zinazowatenganisha.
Akizungumza na Mwanaspoti, Riyama amesema watu wamekuwa na tabia ya kuzungumza kuhusu maisha yao bila kuwa na uhakika, lakini yeye haoni sababu ya kuingia kwenye mabishano.
“Watu wakiamua kusema lao wanasema bila kuwa na uhakika wa jambo, hivyo wakiwa wanasema mimi huwa naangalia tu, kwani sina muda wa kujibizana nao kuhusu maisha ya ndoa yangu,” amesema Riyama.
Kauli hiyo imekuja baada ya kuonekana tena akiwa na Mysterio, huku ikifuatia taarifa zilizowahi kusambaa kwamba wawili hao wameachana.
Riyama, ambaye amekuwa kwenye ndoa hiyo kwa miaka 10, anaonekana kuchagua kuwaacha watu waendelee kusema yao huku yeye akiendelea na maisha yake bila kujibu kila kinachozungumzwa kuhusu ndoa yake.