Jamaa Kigeugeu lakini pesa kibao
MWANDISHI WETU KIGEUGEU ndiyo singo ya Jaguar inayotamba kila kona ya Kenya huku Waziri Mkuu, Raila Odinga akiwa shabiki wake mkubwa lakini msanii huyo ametaja vyanzo vyake vya utajiri. Msanii huyo ambaye katika siku za karibuni amekuwa akishiriki hafla mbalimbali za kuchangia misaada ya chakula kwa wahanga, alisema ana biashara nyingi lakini kubwa ni tatu. "Nina gereji za magari, gari za kukodi na kampuni za ulinzi,"alisema msanii huyo ambaye alidai kuwa huwa hatumii ulevi. "Nina biashara nyingi halafu kusota kumenifanya nijue kutunza fedha sana. Sina matumizi mabaya. Natumia siku tano kufanya biashara zangu shoo nafanya wikiendi."