Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Penalti zatawala Atletico Madrid, Arsenal zikitoshana nguvu

Muktasari:

  • Wakiwa wanacheza nusu fainali ya pili mfululizo ya Uefa kwa mara ya kwanza katika historia yao, Arsenal walijua wanahitaji mwanzo imara wakiwa Hispania, ambako Atletico hawajafungwa katika michezo yao sita iliyopita ya hatua ya mtoano ya michuano hii dhidi ya timu za England, ikishinda tatu sawa na sare.

ATLETICO Madrid na Arsenal wametoka sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya UEFA Champions League uliotawaliwa na penalti.

Wakiwa wanacheza nusu fainali ya pili mfululizo ya Uefa kwa mara ya kwanza katika historia yao, Arsenal walijua wanahitaji mwanzo imara wakiwa Hispania, ambako Atletico hawajafungwa katika michezo yao sita iliyopita ya hatua ya mtoano ya michuano hii dhidi ya timu za England, ikishinda tatu sawa na sare.

Wakiungwa mkono na mashabiki wao wenye hamasa kubwa, kikosi cha Diego Simeone kilipata nafasi ya kwanza ya maana, ambapo David Raya aliokoa kwa ustadi shuti la kupinda la Julian Alvarez na kulipeleka nje ya lango.

Arsenal walijibu vizuri, nahodha Martin Odegaard akazuiwa shuti lake hatari na Johnny Cardoso, kabla ya Noni Madueke kupiga shuti lililokwenda nje akiwa umbali wa mita 25.

Baada ya kushinda mechi tano kati ya sita zilizopita za Uefa ugenini msimu huu sare ikiwa moja, Arsenal waliendelea kutawala mchezo, na juhudi zao zilizaa matunda kabla ya mapumziko wakati David Hancko alipomwangusha Viktor Gyokeres ndani ya eneo la hatari.

Gyokeres alisimama kupiga penalti na kufunga kwa kujiamini dhidi ya Jan Oblak, akifunga bao lake la 19 msimu huu na kuipa Arsenal uongozi kabla ya mapumziko.

Atletico walirejea kipindi cha pili kwa nguvu, Julian Alvarez akipiga mpira wa adhabu uliogonga wavu wa pembeni, huku Ademola Lookman akizuiwa kwa karibu na Raya.

Shinikizo lao lilizaa matunda walipopata penalti baada ya Ben White kushika mpira ndani ya boksi. Alvarez hakukosea alipofunga penalti na kusawazisha.

Atletico walikaribia kuongoza dakika ya 63 wakati Antoine Griezmann alipiga mpira uliogonga mwamba wa juu wa lango.

Licha ya kuendelea kuwa tishio, kumalizia nafasi kwa uzembe kutoka kwa Lookman na uokozi mzuri wa Raya uliifanya Arsenal kubaki salama.

Arsenal walidhani wamepata penalti ya pili baada ya Hancko kumchezea rafu Eberechi Eze, lakini uamuzi huo ulifutwa baada ya ukaguzi wa VAR.

Katika dakika za mwisho, Atletico walishindwa kurejesha makali yao ya ushambuliaji, huku Arsenal wakidhibiti mchezo na kubeba matokeo mazuri kuelekea mchezo wa marudiano Jumanne ijayo huko London Kaskazini.

Kwa upande wa Atletico, wataenda ugenini wakiwa na matumaini makubwa licha ya sare, wakikumbuka wamefanikiwa kusonga mbele katika nusu fainali sita kati ya saba zilizopita kwenye mashindano ya UEFA.