Liverpool yanusurika Newcastle, Iraola akiri kuna kazi
Muktasari:
- Msimu uliopita Liverpool ilipowasili St James' Park, ilishuhudia furaha kubwa baada ya Rio Ngumoha kufunga bao la ushindi dakika ya 100, lakini safari hii hali ilikuwa tofauti kwani penalti ya Szoboszlai iliipa timu hiyo sare.
NEWCASTLE, ENGLAND: Liverpool ililazimika kusubiri hadi dakika ya 99 kupata bao la kusawazisha kupitia mkwaju wa penalti wa Dominik Szoboszlai na kuondoka na sare ya mabao 2-2 dhidi ya Newcastle United, katika mchezo uliompa kocha Andoni Iraola maswali mengi kuliko majibu.
Msimu uliopita Liverpool ilipowasili St James' Park, ilishuhudia furaha kubwa baada ya Rio Ngumoha kufunga bao la ushindi dakika ya 100, lakini safari hii hali ilikuwa tofauti kwani penalti ya Szoboszlai iliipa timu hiyo sare.
Newcastle iliongoza mara mbili, lakini Liverpool haikukata tamaa hadi filimbi ya mwisho na kuibuka na pointi moja.
Kocha wa Liverpool, Iraola ameongeza timu yake haikustahili kupoteza mchezo huo na akafurahishwa na namna wachezaji wake walivyopambana hadi dakika za mwisho.
“Huenda si matokeo uliyokuwa unayataka kabla ya mchezo, lakini hakika tunastahili pointi hii na hata zaidi. Timu haikukata tamaa na tumeokoa pointi moja. Huenda ladha yake ni nzuri zaidi kwa sababu tumefunga dakika ya mwisho,” ameongeza Iraola.
Sare hiyo iliendeleza rekodi ya Liverpool kutopoteza katika mchezo wake wa kwanza wa msimu tangu msimu wa 2012/13, lakini pia ilifichua mapungufu kadhaa kwenye kikosi hicho.
WIRTZ, ISAK WATAKIWA KUONGEZA MAKALI
Macho mengi yalikuwa kwa Florian Wirtz na Alexander Isak, ambao wote walijiunga na Liverpool kwa ada kubwa msimu uliopita.
Isak, ambaye alihamia Liverpool akitokea Newcastle baada ya sakata la muda mrefu la uhamisho, alizomewa kila alipogusa mpira na mashabiki wa timu yake ya zamani.
Mshambuliaji huyo wa Sweden aligusa mpira mara 28 na alionekana kuwa na hamu ya kufanya vizuri, lakini alikosa nafasi nzuri kipindi cha pili ambayo angeweza kuitumia kuifunga Newcastle.
Wirtz alianza vizuri, lakini alitolewa muda mfupi baada ya Newcastle kufunga bao la pili na kufanya matokeo kuwa 2-1.
Mchambuzi wa zamani wa Scotland, Pat Nevin, ameongeza Liverpool bado ina kazi ya kufanya ili kufikia kiwango kinachotarajiwa.
“Unatarajia Liverpool kumaliza angalau ndani ya nne bora msimu huu, lakini leo haikuonekana kama timu ya nne bora. Kuna wachezaji wengine wanaokuja, hivyo huwezi kufanya uamuzi wa mwisho kuhusu msimu wao,” ameongeza.
Nevin ameongeza kuwa Liverpool inahitaji ubunifu zaidi na lazima iwasaidie Wirtz na Isak kuonyesha kiwango chao bora.
GAKPO ATOA UWEZO WAKE
Licha ya Liverpool kuhusishwa na kutaka kuongeza washambuliaji wengine, Cody Gakpo alikuwa miongoni mwa wachezaji bora wa timu hiyo dhidi ya Newcastle na alifunga bao kwa ustadi mkubwa.
Liverpool imekuwa ikihusishwa na wachezaji wa Paris Saint-Germain, Bradley Barcola na Ibrahim Mbaye, huku pia ikiripotiwa kuwa imekataliwa ofa mbili za kumsajili Yankuba Minteh kutoka Brighton.
Endapo Liverpool itafanikiwa kusajili washambuliaji wengine wawili, Gakpo anaweza kuondoka, lakini kiwango chake dhidi ya Newcastle kinaweza kuwapa viongozi wa klabu sababu ya kutafakari upya uamuzi huo.
Pia, mshambuliaji wa Hispania, Victor Munoz, alitoa matumaini baada ya kuingia akitokea benchi na kufanikiwa kuipatia Liverpool penalti iliyosababisha bao la kusawazisha.
IRAOLA AITAKA LIVERPOOL KUONGEZA KIKOSI
Iraola bado anaamini Liverpool inahitaji kuongeza chaguo zaidi kwenye kikosi chake, hasa baada ya baadhi ya wachezaji kushindwa kuonyesha kiwango kizuri.
Mabeki wa pembeni, Milos Kerkez na Jeremie Frimpong, walikuwa na mchezo usioridhisha, huku Liverpool ikiruhusu mabao yote mawili kupitia mashambulizi ya kushtukiza.
Tatizo la kiungo mkabaji pia lilionekana, huku Iraola akimpeleka Alexis Mac Allister mbele ya mabeki baada ya Joe Willock kuifanya Newcastle kuongoza 2-1.
Liverpool sasa imefungwa mabao mengi kupitia mashambulizi ya haraka katika michuano yote kuliko timu yoyote ya Ligi Kuu England tangu kuanza kwa msimu uliopita, ikiwa imeruhusu mabao tisa kwa njia hiyo.
Hata hivyo, Iraola ameongeza ameridhishwa na mambo kadhaa aliyoyaona kutoka kwa timu yake.
“Napenda mambo mengi niliyoyaona kutoka kwa timu. Hakika kuna mambo ya kuboresha, kama suala la kufungwa mabao, lakini nimeona mambo mengi ninayoyapenda. Nimependa nguvu na kasi, hasa wachezaji walioingia kutoka benchi. Tulimaliza mchezo tukiwa na nguvu nzuri kimwili,” ameongeza.
Szoboszlai naye aliahidi Liverpool itaendelea kupambana hadi mwisho.
“Hatutaacha kamwe. Lazima tupambane kila wakati, siku nzima ndani ya dakika 90. Kila aliyeingia kutoka benchi alitoa mchango. Tunahitaji kikosi kizima na lazima tuwe tayari,” ameongeza.
Liverpool imeanza msimu kwa pointi moja, lakini mchezo huo umeonyesha wazi kuwa Iraola bado ana kazi ya kuboresha ubora na kina cha kikosi chake.