Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Waendesha baiskeli 100 kukiwasha Arusha

Arusha. Zaidi ya waendesha baiskeli 100 mkoani  Arusha wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya baiskeli yatakayofanyikwa Aprili 22 jijini hapa.
Akizungumzia mashindano hayo, Muandaaji wa mbio hizo za baiskeli, Linus Katabalo  amesema kuwa, lengo la mashindano hayo ni kumpongeza Nabii Mkuu GeorDavie kwa kazi kubwa anayoifanya ya kusaidia jamii katika masuala mbalimbali ya maendeleo.
"Tumeamua kuandaa  mashindano haya kwa lengo la kumpongeza Nabii Mkuu kwa namna ambavyo anasaidia jamii pamoja na kusaidia vijana bila kujali kabila wala dini hilo ni jambo kubwa na linahitaji kupongezwa na kuungwa mkono kwani ni watu wachache wenye moyo  huo," amesema Linus.
Amesema  mashindano hayo yataanzia barabara ya Haki iliyopo Kisongo na kutumia kilometa 45 baada ya mashindano hayo washindi mbalimbali watapatiwa  zawadi.
Aidha ameongeza kama vijana wanatambua na kudhamini  mchango  mkubwa ambao unaofanywa na Nabii Mkuu kwa jamii inayomzunguka  hivyo hawana budi  kushirikiana  naye  na kuendelea kumuunga  mkono kwa juhudi zake hizo.
Kwa upande wa waendesha baiskeli hao, Mohamed amesema  jambo linalofanywa na Nabii Mkuu GeorDavie ni jambo kubwa sana kwani anasaidia watu kujikwamua kiuchumi na kuondokana na changamoto mbalimbali za maisha jambo ambalo ni kubwa sana na linahitaji kupongezwa na kuungwa  mkono kwa kiwango cha juu.

Mwendesha baiskeli  mwingine Ezekiel Mwakyoma amewataka vijana wengine kujitokeza kwa wingi kushiriki mashindano hayo.