Dakika 28 za moto DJ Ally B akipagawisha Yanga Day
Muktasari:
- Ally B aliingia kwenye shoo hiyo akiwa amevalia kipensi cheusi huku akiwa bila fulana akipiga nyimbo tofauti zenye mchenganyiko wa Bongo Fleva na Singeli.
DJ Ally B amefanya shoo kali kwenye kilele cha Yanga Day akifanya shoo kali ya kupiga muziki, kucheza na kuweka vichombezo.
Ally B aliingia kwenye shoo hiyo akiwa amevalia kipensi cheusi huku akiwa bila fulana akipiga nyimbo tofauti zenye mchenganyiko wa Bongo Fleva na Singeli.
Achana na kupiga muziki huo, Ally B ameonyesha umahiri mkubwa wa kucheza akiondoka kwenye steji na kuwafuata mashabiki pembeni ya majukwaa na kuimba nao.
Ally B ametumia dakika 28 kupiga shoo hiyo kali kwenye Uwanja wa Uhuru, akipiga jumla ya nyimbo 19 tofauti.
Wakati wote Ally B akiwa kwenye shoo hiyo, mashabiki wengi majukwaani wamekuwa wakipagawa kwa furaha wakicheza na kuimba kwa kufuatisha nyimbo hizo.
Yanga imekuwa ikimtumia DJ Ally B kwa mara ya tatu sasa mfululizo kwenye matamasha ya namna hii na hata baadhi ya mechi za kimataifa.
Mara baada ya Ally B kumaliza shoo hiyo, mashabiki walionekana kukaa chini kwenye viti wakipumzika baada ya dakika 28 za moto za kucheza kwa vaibu kubwa.