Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ngoma sita Yanga inazocheza nazo Zenji

YANGA Pict


YANGA tayari ipo visiwani Zanzibar kujiandaa na mechi ya mwisho ya Kundi B ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi y JS Kabylie ya Algeria itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa New Amaan, visiwani humo, huku wawakilishi hao wa Tanzania wakihitaji ushindi usiopungua 2-0.


Yanga inayoshika nafasi ya tatu kwa sasa ikiwa na pointi tano katika msimamo wa kundi hilo linaloongozwa na Al Ahly ya Misri yenye pointi tisa, ikifuatiwa na As FAR Rabat ya Morocco yenye pointi nane, huku Kabylie ikiburuza mkia na alama zao mbili kila moja ikicheza mechi tano.


Hata hivyo, licha ya Yanga kuhitaji ushindi usiopungua mabao 2-0, lakini ni lazima ipige dua sana na kuwaombea mabaya As FAR ugenini mbele ya Al Ahly ili kujihakikishia tiketi ya kucheza robo fainali kwa mara ya pili ndani ya misimu mitatu ya michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa.

Msimu uliopita Yanga ilikwama kwenda hatua hiyo kwa kumaliza katika nafasi ya tatu nyuma ya Al Hilal ya Sudan na MC Alger ya Algeria na kufuatiwa na TP Mazembe iliyomaliza mkiani mwa Kundi A, ikiwa ni msimu mmoja tangu Yanga ilipocheza robo fainali na kutolewa na Mamelodi Sundowns.

Hakuna kitu kingine ambacho Yanga itakihitaji zaidi ya kushinda mbele ya Kabylie lakini kuna mambo matano yanayohitajika ili hesabu za mabingwa hao wa Tanzania zikae sawa na kutinga hatua ya robo fainali.


NOND 03

KUSHAMBULIA NA KUTUMA NAFASI

Yanga haina cha kupoteza katika mechi hiyo ya Jumapili, hivyo lazima ishuke uwanjani na akili ya kushambulia zaidi na si kujilinda sana kama ambavyo ilifanya katika mchezo uliopita, kocha Pedro Goncalves anatakiwa kuwa na mbinu za hali ya juu kuhakikisha wanatengeneza nafasi za kutosha.

Katika mechi ambazo Yanga ilishindwa kutengeneza ushindi haikuwa na makali katika kushambulia na hata mechi pekee iliyoshinda dhidi ya AS FAR Rabat kwenye uwanja huo wa Amaan, ilicheza kwa kushambulia vizuri hesabu ambazo zinatakiwa kurudiwa na Goncalves.

Washambuliaji wa Yanga, iwe ni Depu, Prince Dube au Clement Mzize aliyerejea uwanjani kutoka majeruhi, ni lazima watumie kila nafasi wanazotengenezewa na wenzao kutumbukiza mpira wavuni, kwa sababu ni mechi inayohitaji mabao mengi kabla ya kusikilizia matokeo ya Cairo.


NOND 05

UPANGAJI KIKOSI

Yanga ina changamoto nyingine hapa, bado upangwaji wa kikosi chao unatakiwa kuwa sawasawa hapa. Katika mchezo uliopita ilianza na mshambuliaji mmoja, Laurindo Aurelio ‘Depu’, huku Prince Dube akianzia benchini.

Goncalves anaweza kuanza na mfumo wa 4-4-2 ambao utampa nafasi ya kuwa na washambuliaji wawili watakaowasumbua wapinzani. Pedro anaweza kuanza na Dube pamoja na Depu, lakini akawa na viungo wenye uwezo wa kuharakisha mashambulizi sambamba na wengine wawili wanaoweza kuutafuta mpira.

Katika eneo la ulinzi anatakiwa kuwa na mabeki wawili wanaojua pia kusukuma mashambulizi mbele akiwa na mabeki wawili wa kati badala ya wale watatu ambao alikuwa anaanza nao nyuma akiwa na hesabu za kujilinda zaidi.

Habari njema kwa Yanga ni kwamba Mzize ameonyesha matumaini makubwa ya kurejea baada ya kucheza mchezo uliopita kwa dakika 10 za mwisho ambapo Goncalves hawezi kumuanzisha lakini anaweza kumuongezea muda kipindi cha pili akihofia anaweza kurudi kwenye majeraha.

Kabylie ndio timu ambayo imefunga bao moja tu katika kundi hilo ndani ya mechi tano huku Yanga ikiwa na nafuu kidogo ya kufunga mawili, Waalgeria hao inawezekana hawafungi lakini pia wanajua kujilinda wakiwa na sare tatu zisizo na mabao tena mchezo mmoja ikifanya hivyo dhidi ya Yanga ikionyesha kwamba inaweza kuwa imara kwenye ulinzi.

Yanga lazima wachezaji wake watakaocheza mchezo huo wawe na nguvu ya kuwalazimisha Kabylie kufanya makosa mengi ili kupata nafasi ya kukamilisha malengo yao ya kutafuta ushindi Jumapili pale Uwanja wa Amaan.

Allan Okello anatajwa kuwa mtamu akicheza kama namba 10, hivyo Pedro ana hiari ya kupangua kikosi hicho iwapo anataka matokeo mazuri zaidi, kwani katika mechi iliyopita Pacome Zouzoua alipotea mapema na kama angemtoa na kumsogeza Okello kati kutoka pembeni pengine ingeleta manufaa.

NOND 01

MABAO MATATU MUHIMU

Kutokana na umuhimu wa pambano hilo la mwisho ni wazi vichwani mwa wachezaji wa Yanga wanatakiwa kuwaza kutengeneza ushindi wa mabao yasiyopungua matatu ili kujiweka pazuri dhidi ya hesabu za vikokotoo, huku wakisubiri matokeo ya mechi ya Misri kati ya Al Ahly na AS FAR.

Yanga ikishindwa kupata ushindi wa namna hii inaweza kuwa ngumu kwao kutinga robo kutokana na namna hesabu zilivyo kwa FAR Rabat ambaye anawania naye nafasi ya kwenda robo.

Kwani katika mechi zote tano za awali, Yanga haijafunga zaidi ya bao moja katika mechi moja, ilianza na ushindi wa 1-0 v AS FAR kisha ikatoka suluhu kabla ya kulala 2-0 kwa Al Ahly na sare ya 1-1 waliporudiana na kupoteza ugenini FAR.

Simba waliopo Kundi D na ambao wanaonekana kuwa na msimu mbaya zaidi na kuchekwa.

Ndio, Simba kwa sasa ina pointi mbili na kesho itavaana na Stade Malien ya Mali iliyotinga robo fainali mapema ambapo kama Mnyama atapata ushindi wa kwanza nyumbani kwa msimu huu, itawafanya wafikishe pointi tano kama ilizonazo Yanga iwapo vijana wa Jangwani watachemsha.

YANG 01
YANG 01

PEDRO KASEMA

Kocha Pedro Goncalves amesema mapema kwamba mechi ya keshokutwa sio nyepesi hata kama JS Kabylie haijafanyi vizuri hivyo ni muhimu kwao kupambana.

Amesema kupata ushindi wa pili nyumbani utakaifanya Yanga imalize pazuri bila kuangalia matokeo ya wapinzani wao.

“Ni mechi ngumu na muhimu kwetu, tunahitaji kushinda kwanza kisha ndipo tujue kitatukuta nini, tulishakosea hesabu mechi zilizopita, lakini hakuna muda wa kujadili hili ni wakati wa kujipanga kupata matokeo mzuri nyumbani mbele ya mashabiki wanaotusapoti siku zote,” amesema Pedro.