Hukumu ya namba EPL ikirudi wikiendi
Muktasari:
- Leo Jumamosi zinapigwa mechi saba, kesho Jumapili mbili na keshokutwa Jumatatu kutakuwa na mchezo mmoja kukamilisha raundi hiyo inayotarajiwa kuwa na matokeo ya kushangaza kama tatu zilizotangulia.
MANCHESTER, ENGLAND: ZINAPIGWA mechi za raundi ya nne ya Ligi Kuu England (EPL) wikiendi hii, ambapo wakubwa wote watakuwa mzigoni kusaka alama tatu baada ya kumalizana na michezo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyopigwa katikati ya wiki wote wakiondoka na ushindi dhidi ya wapinzani waliokutana nao.
Leo Jumamosi zinapigwa mechi saba, kesho Jumapili mbili na keshokutwa Jumatatu kutakuwa na mchezo mmoja kukamilisha raundi hiyo inayotarajiwa kuwa na matokeo ya kushangaza kama tatu zilizotangulia.
Ushindi wa Arsenal wa kugeuza matokeo dhidi ya Chelsea Jumapili iliyopita unamaanisha kwamba sasa kuna timu mbili pekee zenye rekodi ya kushinda kwa asilimia 100 baada ya mechi tatu. Manchester City wako sawa na Arsenal wakiwa na pointi tisa, lakini kwa kuwa mchezo unaofuata ni Derby ya Manchester, kikosi cha kocha Enzo Maresca kitakuwa na kazi kubwa ya kuendelea na rekodi yake nzuri.
Chini ya msimamo, Coventry City na Fulham ndizo timu pekee ambazo bado hazijapata hata pointi moja. Coventry City pia ni miongoni mwa timu tatu ambazo bado hazijafunga bao, pamoja na Aston Villa na Tottenham Hotspur.
Kwa kuwa hakuna mchezo wa mapema leo Jumamosi, ratiba inaanza moja kwa moja kwa michezo mitano ya saa 11:00 jioni, ukiwamo wa Aston Villa dhidi ya Nottingham Forest. Villa hatimaye ilipata ushindi wake wa kwanza wa msimu baada ya kuichapa Club Brugge 3-2 katika Ligi ya Mabingwa Jumanne, hivyo kocha Unai Emery atakuwa na hamu zaidi ya kupata pointi tatu katika Ligi Kuu England.
Na katika utabiri mwingi unaoambatana na namba za namna walivyokuta unaipa Villa nafasi ya asilimia 44.8 ya kushinda, ikichagizwa na ukweli kwamba wameshinda kila mmoja wa michezo yao sita iliyopita ya nyumbani dhidi ya Forest katika Ligi Kuu England. Hata hivyo, Villa inaingia katika mechi ya nne bila bao la ligi kwa msimu wa pili mfululizo, huku ikiwa nafasi ya 19 kwa mabao yanayotarajiwa (2.6 xG), nafasi ya 18 kwa miguso ndani ya boksi la wapinzani (45) na nafasi ya 16 kwa xG kwa kila shuti (0.1) katika Ligi Kuu msimu huu.
Forest pia inatafuta ushindi wake wa kwanza chini ya kocha mpya Oliver Glasner, huku ikipewa nafasi ya asilimia 29.2 ya kushinda.
ata hivyo, ni timu tatu pekee zilizotoka sare mara nyingi zaidi katika ligi mwaka 2026 kuliko Forest (10), huku ni Andoni Iraola (33) pekee (aliyekuwa Bournemouth) aliyesimamia sare nyingi zaidi kuliko Glasner tangu alipowasili katika mashindano hayo Februari 2024 (31). Kuna nafasi ya asilimia 26 ya mchezo kuisha kwa sare, ambayo ndiyo nafasi kubwa zaidi ya sare wikendi hii.
Baada ya kuruhusu Newcastle United kusawazisha dakika za mwisho wiki iliyopita, Bournemouth imekuwa timu ya kwanza katika historia ya EPL kuongoza katika michezo yake mitatu ya kwanza ya msimu, lakini haikushinda hata mmoja. Hakuna timu ambayo imewahi kuanza msimu kwa michezo minne ya aina hiyo.
Kikosi cha Marco Rose kilichoifunga Lincoln City katika Kombe la Caraba katikati ya wiki, kitatarajia kupata matokeo dhidi ya Brentford nyumbani, huku kikipewa nafasi ya asilimia 39.4 ya kushinda dhidi ya 35.7 ya Brentford, ingawa kuna nafasi ya asilimia 25 ya sare. Huenda hilo lisiwe jambo la kushangaza. Bournemouth (12) na Brentford (11) ni timu mbili kati ya tatu zilizopata sare nyingi zaidi katika Ligi Kuu England 2026.
Brentford, kwa upande mwingine, haijapoteza katika michezo mitano ya mwisho ya ligi (imeibuka na ushindi mmoja na sare nne), na inaweza kufikisha mfululizo wa michezo sita bila kupoteza chini ya Brentford, baada ya kufanya hivyo mara mbili tofauti msimu uliopita.
Kwa upande mwingine, Chelsea na Hull City zote ziliingia mchezo wa tatu zikiwa na rekodi ya ajabu, ingawa hakuna iliyofanya vyema kwa kuw ana na mwanzo wa asilimia 100, baada ya Blues kufungwa 2-1 na Arsenal na Hull kutoka suluhu na Villa. Ni Chelsea ya Xabi Alonso iliyotoka kuishinda Leeds United 6-3 katika Kombe la carabao katikati ya wiki inayopendelewa Stamford Bridge, ikiwa na nafasi kubwa zaidi ya ushindi katika siku hiyo ya mechi, asilimia 76.1, ikilinganishwa na asilimia 9.5 ya Hull.
Hull haijawahi kushinda katika mechi 18 za ligi ilizocheza ugenini dhidi ya Chelsea (sare 3, kufungwa 15), ikiwa ni timu ambayo imekutana nayo mara nyingi zaidi ugenini katika madaraja manne ya juu bila kushinda.
Huo pia ni mfululizo mrefu zaidi ambao Chelsea imewahi kuikaribisha timu yoyote bila kupoteza katika historia yake ya ligi. Wachezaji wa Alonso wamefunga ndani ya dakika tano za kwanza katika kila mmoja wa michezo yao mitatu ya EPL, na ni Brentford pekee, Septemba/Oktoba 2024 ndiyo iliyowahi kufanya hivyo katika michezo minne mfululizo. Hakuna timu iliyowahi kufanya hivyo mwanzoni mwa msimu.
Hata hivyo, Hull bado haijaruhusu bao msimu huu. Inaweza kuwa timu ya kwanza iliyopanda daraja kuanza msimu wa EPL ikiwa na michezo minne mfululizo bila kufungwa bao.
Ukiachana na hizo, Crystal Palace inapewa asilimia 51.1 ya ushindi na Ipswich Town (asilimia 25.3) zote zina pointi tatu kabla ya kukutana kwenye Uwanja wa Selhurst Park. Baada ya kuanza msimu kwa kufungwa michezo miwili, Crystal Palace ilipata ushindi wa kwanza baada ya kuifunga Fulham 3-2 kwa kugeuza matokeo.
Sasa inaweza kushinda michezo miwili mfululizo EPL kwa mara ya kwanza tangu Desemba 2025, lakini lazima ivunje rekodi mbaya ya nyumbani. Na miongoni mwa zile ambazo zimecheza kila msimu Ligi Kuu England, ni Tottenham Hotspur pekee (saba) ndiyo iliyokusanya pointi chache zaidi nyumbani kuliko Palace mwaka 2026 (11 – ushindi 2, sare 5, kufungwa 4).
Ipswich, kwa upande mwingine, haijapata 'clean sheet' katika michezo 22 ya mwisho ya Ligi Kuu England ikiruhusu mabao 57 katika kipindi hicho, wastani wa 2.6 kwa mchezo. Kocha wake, Gary O’Neil pia hajawahi kuifunga Palace katika majaribio yake matano kama kocha wa ligi hiyo (sare 1, kufungwa 4), huku akipoteza michezo mingi zaidi katika mashindano hayo dhidi ya Manchester United na West Ham pekee.
Na mchezo mwingine unakumbusha Liverpool ilipata ushindi wake wa kwanza chini ya Iraola mara ya mwisho ilipocheza dhidi ya Ipswich, na baada ya ushindi wa mabao 2-1 wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Atletico Madrid, inatarajiwa kupambania mwingine dhidi ya Fulham ambayo bado inatafuta pointi yake ya kwanza chini ya kocha Alvaro Arbeloa. Liverpool imepoteza michezo miwili pekee kati ya 33 iliyocheza nyumbani dhidi ya Fulham katika ligi (ushindi 23, sare 8), hivyo siyo jambo la kushangaza kupewa nafasi ya asilimia 65.5 ya kushinda, leo Jumamosi.
Liverpool imetoka sare katika kila mmoja wa michezo mitatu ya mwisho EPL huko Anfield ikiwa ni mfululizo wake mrefu zaidi bila ushindi katika uwanja huo tangu Desemba 2020 hadi Machi 2021 (sare 2, kufungwa 6), huku nafasi ya mchezo kuisha kwa sare ikitarajiwa kuwa asilimia 18.3.
Na ieleweke kuwa ni mara mbili tu Fulham imewahi kupoteza michezo yake minne ya kwanza katika msimu wa ligi hiyo na katika misimu yote miwili ilishuka daraja. Na sasa inapewa nafasi ya asilimia 16.2 ya kupata ushindi wake wa kwanza. Huo utakuwa mchezo wa kwanza wa Arbeloa wa Ligi Kuu England dhidi ya Liverpool ambayo aliichezea michezo 66 katika mashindano hayo. Hata hivyo, wachezaji wa zamani wa Liverpool waliowahi kuwa makocha katika mashindano hayo wamepoteza michezo yao yote mitano ya ukocha dhidi ya klabu hiyo.
Na baada ya mechi za mapema kukamilika, Tottenham itajaribu kusimamisha mwanzo wake mbaya dhidi ya Everton, ambapo ilipunguza makali ya hali hiyo kwa kupata suluhu dhidi ya Forest wiki iliyopita, lakini bado hakijafunga bao msimu huu. Spurs haijawahi kuanza msimu kwa michezo minne mfululizo bila kufunga katika historia yake ya ligi. Hata hivyo, ilishinda yote miwili dhidi ya Everton msimu uliopita kwa jumla ya mabao 4-0. Pia inaonekana kupewa asilimia 48.2 ya ushindi kabla ya mchezo wa leo, huku Everton ikiwa na 27.1 na asilimia 24.7 ikiwa ni sare.
Everton haijapoteza katika ligi msimu huu (ushindi 1, sare 2), huku ikifunga mabao ya kusawazisha katika muda wa nyongeza katika michezo yake miwili iliyopita. Hata hivyo, haijashinda katika michezo yake sita ya mwisho ya ligi ugenini, ikibadilishana kati ya kupoteza (mara tatu) na sare (mara tatu) katika kila mchezo. Mara ya mwisho ilicheza ugenini ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Bournemouth.
Ratiba ya leo Jumamosi itahitimishwa na mchezo kati ya Sunderland na Arsenal, ambao Arsenal itataka kuendeleza rekodi ya asilimia 100 ya ushindi baada ya kuirarua bao 1-0 Napoli Jumatano kwenye Ligi ya Mabingwa UIaya.
Kwa asilimia 65.1 inazopewa, Arsenal ndiyo timu inayotabiriwa zaidi kushinda ugenini wikendi hii. Arsenal imepoteza mchezo mmoja pekee kati ya 14 ya mwisho ya ligi iliyokwenda kucheza Sunderland (ushindi 8, sare 5), ingawa ilitoka sare ya mabao 2-2 katika uwanja huo msimu uliopita.
Iwapo itashinda, Arsenal itakuwa imeshinda michezo yake minne ya kwanza ya msimu wa EPL kwa mara ya sita katika historia yake.
Sunderland, inayopewa nafasi ya asilimia 13 ya kushinda, imeifunga Arsenal mara moja pekee katika michezo yake 29 ya mwisho ya Ligi Kuu England (sare 10, kufungwa 18), lakini imeshinda miwili ya mwisho ya ligi nyumbani na yote dhidi ya timu kutoka London, Chelsea na Fulham.
MECHI ZINGINE
Wakati changamoto za Villa na Tottenham katika kufunga mabao hazijawazuia kupata pointi, Coventry City haina pointi, ushindi wala bao baada ya michezo mitatu kuelekea mchezo wa Jumapili dhidi ya Brighton. Katika historia ya EPL, Crystal Palace 2017-18 ndiyo iliyowahi kupoteza michezo minne ya kwanza ya msimu bila kufunga bao, ingawa hatimaye ilimaliza msimu huo ikiwa nafasi ya 11.
Timu hiyo imeanza msimu mmoja pekee katika historia yake ya ligi kwa kupoteza michezo minne mfululizo, ambayo ilikuwa katika msimu wake wa kwanza wa Football League 1919-20. Kikosi cha Frank Lampard hakipewi nafasi kubwa dhidi ya Brighton, huku kikipewa nafasi ya asilimia 25.1 ya kushinda dhidi ya asilimia 50.7 ya Brighton, huku asilimia 24.2 iliyobaki ikiwa ni sare. Brighton imepoteza michezo yake mitatu ya mwisho ya ligi ugenini. Hata hivyo, imepoteza mmoja pekee kati ya 14 ya mwisho dhidi ya timu zilizopanda daraja (ushindi 7, sare 6).
Macho yote yataelekezwa Manchester Jumapili, wakati Man City itakapojaribu kuendeleza mwanzo wake bora wa ligi dhidi ya Man United.
City ndiyo inayopewa nafasi ya asilimia 44.2 ya kushinda dhidi ya asilimia 31.6 ya United, lakini City imeshinda mchezo mmoja pekee kati ya minne ya mwisho ya ligi dhidi ya Mashetani Wekundu (sare 1, kufungwa 2). United ina rekodi nzuri nyumbani chini ya Michael Carrick, ikiwa imeshinda michezo tisa kati ya 10 ya ligi huko Old Trafford tangu alipopewa jukumu Januari, mwaka huu (ikipoteza 1).
Pia anaweza kuwa kocha wa tatu katika historia ya klabu hiyo kushinda michezo yake miwili ya kwanza ya ligi dhidi ya City ambayo inataka kushinda michezo yake yote minne ya kwanza ya msimu wa ligi kwa mara ya saba, jambo ambalo litaifanya kuwa timu iliyofanya hivyo mara nyingi zaidi katika historia ya mashindano hayo (Chelsea pia mara 6).
Ratiba itahitimishwa Jumatatu, Elland Road ikiwa mwenyeji wa mchezo kati ya timu mbili ambazo bado hazijapoteza na zote zina pointi tano; Leeds United na Newcastle United. Kikosi cha Leeds United kimepoteza mchezo mmoja kati ya 12 ya mwisho ya ligi (ushindi 5, sare 6) tangu msimu uliopita, na kinaweza kumaliza michezo minne ya kwanza ya msimu bila kupoteza kwa mara ya nne baada ya kufanya hivyo 1995-96, 1998-99 na 2001-02.