Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Fadlu si wa kwanza, ila kuna darasa tosha!

NONDO Pict

Muktasari:

  • Hii imetokana na aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Fadlu Davids na wasaidizi wake kadhaa aliotua nao kutoka Raja Casablanca wakati anaajiriwa Msimbazi mwaka mmoja na ushei kuondoka ghafla klabuni.


MABOSI wa Simba huenda kwa sasa wapo bize kwa ajili ya kupitia na kusoma kwa umakini CV na maombi ya makocha wanaowania ajira klabuni hapo.


Hii imetokana na aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Fadlu Davids na wasaidizi wake kadhaa aliotua nao kutoka Raja Casablanca wakati anaajiriwa Msimbazi mwaka mmoja na ushei kuondoka ghafla klabuni.


Tetesi za Fadlu kuondoka Simba zilianza mapema mara baada ya kumalizika kwa msimu uliopita ambao aliiwezesha timu hiyo kufika fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, kutokana na kumaliza mkataba wa awali kumalizika.

Hata hivyo, mambo yaliwekwa sawa na kocha huyo kuongezwa mkataba mwingine mpya alioanza kuutumikia lakini ghafla baada ya Ngao ya Jamii zilienea taarifa kwamba kocha huyo asingerudi kutoka Botswana, ambako timu hiyo ilienda kucheza mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu.

Licha ya viongozi wa klabu hiyo kuuma maneno kwamba kocha huyo bado yupo sana, ila vyanzo vilishanusa kwamba jamaa alikuwa anarudi alikotoka kwa maana ya Raja Casablanca kabla ya Fadlu mwenyewe kuaga na ndipo mabosi wa Simba kutoa taarifa kwamba wamekubaliana kuachana.

NONDO 01

Kwa sasa Simba itakuwa chini ya Seleman Matola kwa kusimamia Ligi Kuu, wakati Hemed Suleiman ‘Morocco’ akipewa kibarua cha kuisimamia katika mechi ya marudiano ya CAF kutokana na Matola kuonyeshwa kadi nyekundu katika mechi iliyopita.

Ni wazi mashabiki wa Simba wamevurugwa kwa kuondoka kwa Fadlu na wenzake, lakini kuna jambo ni lazima walijue mapema.

Katika mchezo wa mpira wa miguu mabadiliko ya makocha hayawezi kuepukika kutokana na mazingira halisi ya mchezo wenyewe ulivyo. Wapo wanaoamini suala la kutimuliwa makocha ni kama utamaduni katika soka kiasi cha kuibuka kauli maarufu isemayo; ‘makocha huajiriwa ili watimuliwe.’

Kwa maana kwamba hakuna kocfha wa milele katika klabu au timu yoyote, wanakuja na kuondoka kutokana na mahitaji na zama zilivyo.

NONDO 02

Klabu inaweza kuajiri makocha inaowahitaji kwa wakati huo kulingana na malengo waliyojiwekea na pale ikitokea yasipofikiwa, basi uongozi huwa wanalazimika kutafuta suluhisho wakiangalia kikosi walichonacho na kile wanachokipata kiwanjani.

Kama wasifu wa wachezaji wanaridhika nao, basi huwa wanarudi kuangalia benchi la ufundi na iwapo watabaini kuna tatizo watalazimika kubadilisha kwa kuajiri watu wengine na hiyo imekuwa ikishuhudiwa mara nyingi katika klabu nyingi iwe hapa nchini au zile za kimataifa.

NONDO 03

Lakini hata kwa upande wa makocha nao huzitumia klabu kutengeneza wasifu wao hasa pale wanapofanikiwa kufikia malengo au hata kuvuka, kwa kupata ofa kubwa kutoka klabu zenye nguvu kiuchumi, ambapo huwa ni vigumu kuzikataa.

Mwisho wa yote ni kwamba makocha wanafanya kazi kwa kuamini kuna siku tutapata zaidi, hivyo ikifikia hizo nyakati sio rahisi kuzikataa kama ilivyowahi kumkuta Sead Ramovic aliyeiacha Yanga na kwenda CR Belouizdad ya Algeria.

Ni sawa na ilivyomkuta Zoran Maki aliyeiacha Simba katika kipindi kifupi na kwenda Al Ittihad na hata kilichotokea kwa sasa za Fadlu na dili lililomrudisha Raja, kwa kutumia kipengele cha kuvunja mkataba na timu kulazimika kutafuta kocha mwingine. Na hapa linakuja suala la klabu zetu kuwekeza kiuchumi ili wakati mwingine kuchuana na hizi klabu kubwa ‘zinazovua baharini’ zitakavyo.

Na hakuna kitu kibaya kama kama mabadiliko ya makocha kufanyika mwanzoni au katikati ya msimu, licha ya ukweli kwamba mabadiliko ya makocha hayana wakati sahihi, ila mwanzoni mwa msimu yanasumbua sana sababu makocha wengi wanakuwa ndio wameanza msimu na klabu zao.

NONDO 04

Hivyo kuwapata gharama huwa kubwa japo mabadiliko huja na chanya au hasi na hapo ndipo mazungumzo huja kutokana na nini kimetokea baada ya mabadiliko bila kujali muda yalipofanyika.

Ujio wa kocha mpya hutegemea msingi ulioachwa na aliyeondoka hasa alienda timu gani wakati wa maandalizi ya msimu mpya

Mbali na kuwa na wachezaji wenye ubora kama nyenzo za kumwezesha mwalimu mpya kuifanya kazi yake vizuri, ila maeneo muhimu anayohitaji (utimamu wa mwili, akili, saikolojia, kimbinu na kijamii kwa lugha ya mpira physically and mentally fitness, tactical, technique, psychology and social).

Haya ni maeneo matano ambayo kocha anayekuja akiyakuta yako vizuri kazi yake inaweza kuwa nyepesi, sababu atakuwa akifanyia kazi utendaji kazi wa kila mchezaji kiwanjani kulingana na yale matukio matano ya mchezo.

Pia kwa namna anavyotaka timu yake iyatafsiri ndiko kunapopatikana utofauti baina ya kocha mmoja na mwingine.

Hivyo tunakubaliana kwamba hakuna wakati sahihi wa kubadilisha kocha kutokana na namna timu zilivyofanikiwa baada ya mabadiliko ya benchi au namna timu zilivyoharibikiwa baada ya mabadiliko.

Mabadiliko chanya ni kila mchezaji kujiona ana nafasi sawa na wengine katika kumshawishi kocha mpya, hivyo kipindi hiki kifupi kocha anaweza kufanikiwa kushinda michezo yake. Kitaalamu, kipindi hiki wanakifananisha na kipindi cha mwezi mmoja baada ya ndoa (honeymoon).

Takwimu zinaonyesha mara nyingi mabadiliko huwa na matokeo chanya hii hukadiriwa michezo mitatu hadi mitano.

Hasi ni kuwapoteza baadhi ya wachezaji kutokana na kutokubaliana na mbinu za kocha mpya aliyekuja au kocha kutowahitaji katika mipango yake kulingana na uchezaji wao bila ya kujali nafasi waliyokuwa nayo awali.

Yote kwa yote mabadiliko yasiyokuwa ya lazima sio ya kuyapa nafasi kwani yanatibua mipango ya timu na kuyumbisha kwa muda hasa pale kocha anaposhindwa kukliki kwa wachezaji. Tujifunze!