Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Nitaanza na mambo sita

Sugu

SAMSON MFALILA BAADA ya ushindi wake wa kishindo wa kutwaa kiti cha ubunge cha Jimbo la Mbeya Mjini, muasisi na mwanaharakati za muziki wa Bongo Flava, Joseph Mbilinyi `Sugu' ameanika mambo makubwa sita atakayopigania bungeni. Sugu amezua gumzo kutokana na kitendo chake cha kupigania ubunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kumshinda mwalimu wake wa zamani wa sekondari. Kinyume cha matarajio ya wengi alimshinda mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Benson Mpesya, ambaye alikuwa anatetea kiti chake na katika mahojiano maalumu na gazeti la Mwanaspoti jana Jumatatu, Sugu ameanika ajenda zake sita. Kutumikia wananchi wa jimbo lake Sugu, ambaye pia anajulikana kwa majina ya utani ya `Mr II' au `II Proud', anasema asilimia 99 ya ajenda yake itakuwa kutatua matatizo ya wananchi wa Mbeya, ambao wana changamoto nyingi. Msanii huyo amewashukuru wananchi wa Mbeya kwa kuwa na imani naye na kuahidi kushughulikia matatizo yao ya barabara, elimu na afya katika kipindi cha miaka mitano ya ubunge. Sheria ya Haki Miliki Anasema itakuwa ni sehemu kubwa ya majukumu yake lakini kuna mambo, ambayo angependa ayafanyie kazi ili asaidie kutatua matatizo ya sanaa ya muziki wa Bongo Fleva, ambao anakiri umemtoa kimaisha. Sugu anasema sheria ya Haki Miliki ina upungufu mkubwa unaofanya iwe ngumu kudhibiti wizi wa kazi za wasanii. Anatolea mfano wa adhabu zinazotolewa kwa wale wanaokamatwa wakidurufu kazi za wasanii kuwa hazijawekwa bayana. "Unajua bwana mwandishi hii sheria inaeleza adhabu ya juu tu (maximum' penalt) lakini haizungumzii adhabu ya chini (mininum penalt). Hii sheria inaeleaelea tu. "Hii inafanya kwa mfano mtu inapotokea mtu amejaza lori aina ya Fuso kazi za wasanii zenye thamani ya Sh. milioni 10 anaweza kutozwa faini ya sh. 200,000. Sheria hii haiko wazi," anaeleza Sugu, ambaye anahesabiwa kati ya waasisi wa Bongo Fleva kiasi cha kufikia kuitwa `Nyerere wa Rap'. Anataka Cosoto ipewe meno Sugu anasema angependa kuona Taasisi ya Kusimamia Haki Miliki (Cosota) ikiimarishwa ili iweze kuwajibika vizuri. Anadai Cosota kwa sasa ni taasisi ndogo kuweza kusimamia kazi za wasanii nchi nzima. "Moja ya mambo nitakayoshughulikia nikifika mjengoni (bungeni) ni kuona Cosota inapewa meno. Unajua tunafanya biashara nchi nzima lakini Cosota inayotakiwa kulinda kazi zetu hawana vitendea kazi vya kutosha na hata rasilimali watu," anaeleza Sugu, ambaye tangu ameanza mwaka 1994 amefyatua albamu 10. Anasema muziki unalipa kama wezi wa kazi za wasanii watadhibitiwa na kuongeza yeye alifanikiwa kimuziki baada ya kuamua kusimamia kazi zake mwenyewe na kuuza nakala zaidi ya 40,000 za albamu ya `Ndani ya Bongo' mwaka 1996. TRA waweke alama kwenye kazi za wasanii Sugu anapendekeza kuwekwa kwa alama au stika za Mamlaka ya Kukusanya Mapato ya Kodi (TRA)kwenye kazi za wasanii ili kudhibiti wizi. Anatetea utaratibu huo kuwa ni mzuri kwani utasaidia Mamlaka ya Kukusanya Mapato ya Kodi (TRA) kuongeza wigo wa mapato na utadhibiti wenye tabia ya kudurufu kazi za wasanii. Anadokeza kuwa aliwahi kushirikina na wasanii wengine wa Bongo Fleva na kupeleka mapendezo serikali tangu wakati wa uongozi wa awamu ya tatu nchini ya Benjamin Mkapa. "Tulipeleka maombi yetu mwaka 1995 kwenye Wizara ya Viwanda na Biashara na tuliambiwa maombi yetu yalikubaliwa lakini kukawa kuna urasimu. Kipindi Rais Jakaya Kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005 tulipeleka tena maombi yetu, Waziri wa wakati ule Nazir Karamagi alikubaliana na ombi letu na akasaini. "Kilichobaki ilikuwa kuchapishwa kwenye Gazeti la serikali ili iwe sheria," anaeleza Sugu, ambaye anaongeza baada ya kufikia hatua hiyo walikuja kutaarifiwa faili lao liliibiwa kutoka meza ya Karamagi. Mabadiliko ya Basata Sugu anasema kuwa Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) linafanya kazi zake kizamani. Anaona linahitaji kufanyiwa mabadiliko kimuundo ili kufanya vizuri kazi zake za kusimamia na kuendeleza sanaa. Anasema kuna haja ya baraza hili kusambazwa nchi nzima kwani haoni mantiki ya msanii anayetoka mkoani kufunga safari Dar es Salaam kwa ajili ya kujisajili na anaeleza kuwa sanaa nchi nzima sasa inakuwaje Basata iwe Dar es Salaam pekee. Kuunganisha wasanii Sugu anaeleza itakuwa ngumu kwa wasanii kupigania haki zao bila ya kuwa kitu kimoja na ametaka wasanii hao kuwa na chombo cha kuwateta na atapigania kufufuliwa kwa Chama cha Wasanii wa muziki wa Kizazi Kipya (Tuma). Anaeleza kuwa chama hicho kilisajiliwa mwaka 2004 lakini kilishindwa kuibuka kutokana na wasanii wenyewe wa Bongo Fleva kukosa ushirikiano. Anasema atashirikiana na wabunge wengine kutetea wasanii lakini nao wanatakuwa kuwa kitu kimoja. Sugu anasema kitendo cha wasanii kukosa umoja ndio maana hata Rais Jakaya Kikwete alipotoshwa wakati alipotaka kusaidia wasanii wa Bongo Fleva. "Rais Kikwete kwa nia njema alitaka kutusaidia lakini kuna watu wakampotosha kuwa eti wasanii tunataka studio . "Kaka studio ziko kibao mtaani hadi zinakosa wasanii wa kurekodi," anasema Sugu, ambaye anamshauri Rais Kikwete kutengeneza mazingira mazuri ya wasanii kufanya kazi. Nitaandaa mikutano na matamasha ya kuwaunganisha wasanii. Siwezi kuacha harakati za muziki wa Bongo Fleva," anaeleza Sugu, ambaye amesema hatarudi jukwaani bali ataendeleza harakati za kupigania kuinua maisha ya wasanii ya kutumia njia nyingine. Harakati za kuwania ubunge Sugu hakuona taabu kuwania ubunge kutokana na uzoefu wa kupigania haki hata akiwa msanii wa Bongo Fleva. Anasema amekutana na vikwazo vingi akiwa msanii wa Bongo Fleva na upo mfano wa kupokonywa mradi alioubuni wa kupambana na Ugonjwa wa Malaria. Pia niliona wananchi wanavyoumia wakati kuna vitendo vya rushwa na ufisadi vinavyosababisha maisha kuwa magumu. Sugu anasema alijua atakuwa na kibarua kigumu cha kugombea ubunge kupitia chama cha upinzani lakini kwa kuwa mzoefu wa mapambano akaibuka mshindi bila ya kutumia rushwa. Alieleza mpinzani wake ambaye alikuwa mwalimu wake, alipokuwa Mbeya Day, akimfundisha Historia na Fasihi, alifanya kampeni kwa siasa za maji taka. Alitolea mfano kwa Mpesya kudai hakumaliza alimu yake ya sekondari kwenye shule ya Mbeya Day na pia alimbeza kwa kuvaa suruali kwa mtindo wa Kata-K na kuvaa hereni. Historia Sugu amezaliwa Mei 1, 1978 na kumaliza Shule ya Msingi ya Sisimba iliyoko mjini Mbeya. Alipata elimu yake ya sekondari ya Mbeya Day, ambako aliondoka akiwa kidato cha tatu mwaka 1990 na kumaliza kidato cha nne mwaka 1991 mkoani Mtwara kwenye Shule ya Sekondari ya Sabasaba. Sugu alifanya kazi Kampuni ya Mafuta ya BP kuanzia mwaka 1994-1998. Anasema alianza kuimba rap tangu akiwa shule mwaka 1989 lakini alianza kutambulika rasmi mwaka 1994. Tangu ameingia kwenye gemu ameachia albamu 10 za `Ni Mimi', `Ndani ya Bongo', `Niite Mr Two', Nje ya Bongo', `Milenia', `Muziki na Maisha', `Itikadi', `Sugu', `Ujio wa Mimi' na `Veto'.