Kocha Simeone atoa onyo kali Italia
Muktasari:
Simione alisema kwa sasa mawazo yake ni kuifanikisha klabu hiyo kumaliza kwenye nafasi ya tatu katika ligi hiyo na hafikirii kuhusu hatima ya ajira yake.
Kocha wa Atletico Madrid amesema haoni sababu ya watu kuanza kuhoji kuhusu hatima ya kibarua chake kwenye klabu hiyo, bali wasubiri mpaka msimu huu ukimalizika.
Simione alisema kwa sasa mawazo yake ni kuifanikisha klabu hiyo kumaliza kwenye nafasi ya tatu katika ligi hiyo na hafikirii kuhusu hatima ya ajira yake.
Simione alisema hajui lolote kuhusu klabu ya Inter Milan ambayo inahitaji huduma yake msimu ujao, baada ya kumtimua kocha wao, Stefano Pioli.