Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Trossard aiteka Istanbul, mashabiki wapagawa kumshuhudia

TROSAD Pict

Muktasari:

  • Nyota huyo anatarajia kutambulishwa rasmi leo kwa mashabiki kwenye uwanja wa nyumbani wa klabu hiyo, Tüpraş Stadyumu (zamani Vodafone Park), huku mamia ya mashabiki wenye shauku kubwa wakijitokeza kwa wingi uwanjani kushuhudia tukio hilo la kihistoria.

Kiungo mshambuliaji wa Ubelgiji, Leandro Trossard, amegeuka kivutio kwa mashabiki wa Besiktas jijini Istanbul baada ya kukamilisha usajili wake akitokea kwa mabingwa wa England, Arsenal. 

Nyota huyo anatarajia kutambulishwa rasmi leo kwa mashabiki kwenye uwanja wa nyumbani wa klabu hiyo, Tüpraş Stadyumu (zamani Vodafone Park), huku mamia ya mashabiki wenye shauku kubwa wakijitokeza kwa wingi uwanjani kushuhudia tukio hilo la kihistoria.

Baada ya utambulisho huo wa kifahari uwanjani, Trossard atapata wasaa wa kipekee wa kukutana na mashabiki na kusaini jezi zao kama sehemu ya kuwakaribisha na kuanza safari yake mpya nchini Uturuki. 


Kuondoka kwa Trossard kumeisukuma Arsenal sokoni ambapo tayari imeshaziba pengo lake kwa kumsajili Christos Tzolis.

Ephraim Bahemu amepiga story na shabiki mmoja wa timu hiyo ambaye ameelezea furaha yake na matarajio yake kwa mchezaji huyo.