Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Arsenal, Tzolis ni suala la muda tu

ARSENAL Pict

Muktasari:

  • Mabingwa hao wa Ligi Kuu England wamekuwa wakisaka winga wa kushoto katika dirisha hili la usajili, huku juhudi hizo zikiongezeka baada ya Leandro Trossard kuwa mbioni kuhamia Besiktas kwa ada ya pauni17 milioni mara baada ya kumaliza majukumu yake na timu ya taifa ya Ubelgiji kwenye Kombe la Dunia.

LONDON, ENGLAND: ARSENAL ipo hatua za mwisho kukamilisha usajili wa winga wa Club Brugge, Christos Tzolis, kwa gharama ya pauni35 milioni litakalomfanya kuwa mchezaji ghali zaidi kuwahi kutoka nchini Ugiriki.

Mabingwa hao wa Ligi Kuu England wamekuwa wakisaka winga wa kushoto katika dirisha hili la usajili, huku juhudi hizo zikiongezeka baada ya Leandro Trossard kuwa mbioni kuhamia Besiktas kwa ada ya pauni17 milioni mara baada ya kumaliza majukumu yake na timu ya taifa ya Ubelgiji kwenye Kombe la Dunia.

Kwa mujibu wa taarifa, Arsenal na Club Brugge zipo karibu kufikia makubaliano ya mwisho ya uhamisho wa Tzolis, ambaye aliwahi kucheza Norwich City. Kilichobaki ni idhini ya mwisho kutoka kwa viongozi wa Arsenal ili mchezaji huyo asafiri kwenda London kwa ajili ya vipimo vya afya na kusaini mkataba.

ARS 01

Iwapo dili hilo litakamilika, Tzolis atavunja rekodi ya kuwa mchezaji wa Ugiriki aliyeuzwa kwa ada kubwa zaidi, akimpita Babis Kostoulas, aliyesajiliwa na Brighton kwa karibu pauni30 milioni msimu uliopita.

Hata hivyo, usajili wa Tzolis hautaathiri mipango ya Arsenal ya kumsaka nyota wa Aston Villa, Morgan Rogers, ambaye bado anaendelea kuwa chaguo la kwanza la kocha Mikel Arteta.

Villa haina mpango wa kumuachia Rogers kirahisi na imeweka dau la pauni130 milioni. Endapo Arsenal italipa kiasi hicho, kiungo huyo ataingia kwenye rekodi ya usajili ghali zaidi katika historia ya Ligi Kuu England, sambamba na Alexander Isak wa Liverpool.

Tzolis alikuwa mmoja wa wachezaji bora wa Club Brugge msimu uliopita baada ya kufunga mabao 22 na kutoa asisti 29 katika mechi 52 za mashindano yote.

ARS 02

Pia, alionyesha kiwango kizuri kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, akifunga mabao mawili na kutoa asisti moja katika mechi tisa, ikiwemo dhidi ya Arsenal ambapo Brugge ilipoteza kwa mabao 3-0 katika hatua ya makundi.

Tangu ajiunge na Club Brugge mwaka 2024, mshambuliaji huyo ameweka rekodi ya mabao 43 na asisti 45 katika mechi 108.

Kabla ya kung'ara nchini Ubelgiji, Tzolis alipitia kipindi kigumu akiwa Norwich City, iliyomsajili kutoka PAOK mwaka 2021 kwa ada ya rekodi ya klabu ya pauni11 milioni.

Hata hivyo, maisha yake Carrow Road hayakuwa rahisi baada ya aliyekuwa kocha wa Norwich, Daniel Farke, kuondolewa miezi mitatu tu baada ya usajili wake. Mrithi wake, Dean Smith, hakumpa nafasi kubwa ya kucheza, hali iliyomlazimu kutafuta changamoto mpya kabla ya kurejea kwenye kiwango chake akiwa Club Brugge.