Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

VIDEO: Wazee Stars waongeza mzuka mazoezini

Muktasari:

Mbali na Tino, wengine waliofika kwenye Uwanja wa Taifa ni Iddi Pazi, Hussein Ngulungu, Leopard Tasso, Omary Hussein 'Keegan' na wengineo.

 Story Nyota wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' walioiongoza kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) wameibuka katika mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea kwenye Uwanja wa Taifa jioni hii kwa ajili ya kuwapa hamasa wachezaji kuelekea mchezo wa kuwania kufuzu fainali hizo dhidi ya Uganda Jumapili.

Ujio wa wachezaji hao uliongozwa na mshambuliaji Peter Tino ambaye alifunga bao la kusawazisha nchini Zambia katika sare ya bao 1-1 ambalo liliivusha Stars kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-1 kufuatia ushindi wa bao 1-0 nyumbani Dar es Salaam.

Mbali na Tino, wengine waliofika kwenye Uwanja wa Taifa ni Iddi Pazi, Hussein Ngulungu, Leopard Tasso, Omary Hussein 'Keegan' na wengineo.

Akizungumzia ziara hiyo ya ghafla, Tino alisema inalenga kuwahamasisha wachezaji kwa ajili ya mechi hiyo dhidi ya Uganda "Kikubwa tumefika hapa kuwapa morali wachezaji wafahamu umuhimu wa kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika," alisema Tino