Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kwa Rashford pesa siyo shida, anataka tu kucheza

Rashford Pict

Muktasari:

  • Kocha wa miamba hiyo ya Old Trafford alifichua sababu za kumwacha Rashford ni kutokana na kutokujituma mazoezini na haridhishwi naye.

WANASEMA ukiona cha nini wengine wanawaza watakipata line. Ndicho kilichotokea kwa Marcus Rashford ambaye alikuwa hapati namba kwenye kikosi cha Manchester United na zaidi hakujumuishwa kabisa kwenye michezo ya timu hiyo.

Kocha wa miamba hiyo ya Old Trafford alifichua sababu za kumwacha Rashford ni kutokana na kutokujituma mazoezini na haridhishwi naye.

Hata hivyo, wakati kocha huyo Mreno akikosa imani na Rashford, nyota huyo wa England ameibukia Aston Villa na jana alitarajiwa kucheza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Tottenham wa Kombe la FA na Kocha Mhispania Unai Emery anaamini atakiwasha kutokana na alivyomwona mazoezini.

RASH 05

Sasa unaambiwa nyota huyo aliye kwa mkopo Villa, wala hana presha kwani kuondoka Man United wala hakujamteteresha nje ya uwanja na maisha ndo yanazidi kuwa matamu kutokana na waleti yake na huku ni kwenda tu kupata changamoto mpya kisoka ili kulinda kipaji chake.

Kwa upande wa pesa, kwake siyo shida na ATM inakuchambulia namna nyota huyu anavyopiga pesa kwenye soka na nje ya soka na anavyozitumia ikiwamo kumiliki mali za maana yakiwamo magari ya kifahari.


ANAVYOPIGA PESA

Akiwa Man United alikuwa analipwa mshahara wa Pauni 350,000 kwa wiki na ndiyo huo huo analipwa Villa aliko kwa mkopo, ikiwa ndiyo asilimia kubwa ya kipato chake.

Nyota huyu pia anapiga pesa kutokana na madili ya ubalozi na udhamini kutoka kampuni mbalimbali zikiwamo Coca-Cola, Chevrolet, Burberry na H&M inayojihusisha na mitindo na huuza mavazi ya bei nafuu.

Pia ana mkataba na kampuni inayomiliki migahawa ya McDonald pamoja na wa Nike inayomlipa kwa kuwa balozi wake.

Kutokana na madili hayo ya mikataba, anavuna takribani Dola 20 milioni kwa mwaka na hadi sasa anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia Dola 80 milioni.

RASH 04

NYUMBA

Mwaka 2021, alinunua nyumba ya kifahari yenye thamani ya Pauni 2.8 milioni huko Wilmslow, Cheshire yenye vyumba vitano vya kulala, chumba cha mazoezi, chumba cha sinema na bwawa la kuogelea la nje.

Rashford pia anamiliki nyumba yenye thamani ya Pauni 1.8 milioni huko Bowdon, Manchester, aliyoinunua mwaka 2019 na ina eneo la mazoezi, ukumbi wa sinema, chumba cha kuchezea game na bustani kubwa.


RASH 03

NDINGA

McLaren 765 Long Tail-Dola 382,000

Rolls-Royce Cullinan-Dola 355,000

Rolls-Royce  Black Badge Wraith-Dola 750,000

Range Rover Velar-Dola 89,225

Mercedes C Class Coupe-Dola 48,437

Mercedes GLA 2020-Dola 38,239

Mercedes S Class Coupe-Dola 131,289

Mercedes-AMG A45 -Dola 52,415

Audi RS4 Avant-Dola 84,460

Mercedes-AMG G63-Dola 180,000

Mercedes-AMG GT63 S-Dola 170,000


RASH 01

MISAADA KWA JAMII

Kama sehemu ya mikataba yake na H&M, alizindua kampeni maalum kuhusu utoaji wa chakula na msaada kwa watoto wa jamii maskini.

Mwaka 2020, aliandika barua ya wazi kwa bunge la Uingereza akiwahimiza wanasiasa kuendelea na mpango wa kutoa chakula cha bure kwa watoto wenye uhitaji kutokana na janga la virusi vya corona.

Pia amekuwa akishirikiana na taasisi ya FareShare inayojihusisha na kutoa msaada wa chakula kwenda kwa watu wasiojiweza.


RASH 02

MAISHA BINAFSI NA BATA

Awali alikuwa katika uhusiano wa muda mrefu na Lucia Loi kabla ya kuachana mwaka jana na kuibukia kwa mrembo Grace Rosa Jackson ambaye pia waliachana Desemba mwaka jana. Kwa sasa haijaripotiwa ikiwa yupo katika uhusiano na mrembo yeyote.