Amorim aonyesha hasira zake Man United

Muktasari:
- Man United ambayo ilianza kwa kuongoza kupitia bao la Alejandro Garnacho,i walijikuta nyuma baada ya Glimt kusawazisha na kuongoza kwa mabao ya Hakon Evjen na Philip Zinckernagel.
MANCHESTER, ENGLAND: KOCHA wa Manchester United, Ruben Amorim alionekana kuwa na hasira kutokana na kosa moja ambalo wachezaji wake walikuwa wakilifanya wakati wa mchezo wao wa Europa League dhidi ya Bodo/Glimt.
Man United ambayo ilianza kwa kuongoza kupitia bao la Alejandro Garnacho,i walijikuta nyuma baada ya Glimt kusawazisha na kuongoza kwa mabao ya Hakon Evjen na Philip Zinckernagel.
Baadaye Rasmus Hojlund alisawazisha kabla ya mapumziko kwa shuti kali, kisha akaongeza bao la tatu kwa timu yake katika kipindi cha pili.
Licha ya ushindi huo kulikuwa na makosa mengi ambayo yalisababisha Amorim kuwa na hasira sana hususani katika kipindi cha kwanza.
Kwa mujibu wa ‘The United Stand’, Amorim alikasirika kwa sababu wachezaji wa walishindwa kupeleka mpira pembeni kwa Antony.