Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wananchi mdogo mdogo kwa Mkapa

MASHABIKI wa klabu ya Yanga wameanza kuingia mdogo mdogo katika uwanja wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya kushuhudia mastaa wao wapya leo.

Yanga leo watakuwa na kilele cha Wiki ya Mwaananchi ambayo inatumika kwa ajili ya kuwatambulisha wachezaji wao wa msimu ujao huku wakicheza mchezo wa kirafiki na Vipers kutoka Uganda.

Mwanaspoti ambalo lipo katika Uwanja wa Mkapa limeshuhudia mashabiki wa Yanga wakiingia polepole uwanjani.

Mashabiki hao walikuwa wachache saa 5 asubuhi tofauti na siku zingine za nyuma. katika Tamasha la siku ya Mwananchi.

Hili ni tamasha la nne kwa Wananchi tangu waanze kufanya ikiwa ni sehemu ya kuwatambulisha mastaa watakaoitumikia timu yao katika msimu unaofuata.