Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

TETESI ZA USAJILI BONGO: Sadio Kanoute, JS Kabylie bado kidogo tu

Kanoute Pict
Kanoute Pict

Muktasari:

  • Inadaiwa kuwa, Kocha Abdelhak Benchikha aliyefanya kazi na Putin wakiwa Msimbazi ndiye aliyetoa pendekezo la kiungo huyo wa kimataifa wa Mali asajiliwe katika timu hiyo.

KIUNGO mkabaji aliyetemwa na Simba hivi karibuni, Sadio Kanoute 'Putin' yupo mbioni kutua klabu ya Ligi Kuu ya Algeria, JS Kabylie.

Inadaiwa kuwa, Kocha Abdelhak Benchikha aliyefanya kazi na Putin wakiwa Msimbazi ndiye aliyetoa pendekezo la kiungo huyo wa kimataifa wa Mali asajiliwe katika timu hiyo.

Duru za kispoti zinadai kwamba mazungumzo ya menejimenti ya mchezaji huyo na JS Kabylie yanaendelea vyema na muda wowote Putin ataungana tena na Benchikha katika timu hiyo.

SADIO KANOUTE

Kuzaliwa: Okt 21, 1996

Mahali: Bamako

Nchi: Mali

Urefu: Mita 1.86

Klabu: Huru

Nafasi: Kiungo Mkabaji

Alikopita: Stade Malien, Al Ahli Benghazi na Simba