Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mastaa Yanga watinga na suti kusalimia

BAADA ya kumalizika kwa mechi ya kirafiki ya  Yanga Princess dhidi ya Ilala Queens,  yaliingizwa mataji matatu la Ligi Kuu Bara, Ngao ya Jamii na Kombe la Shirikisho la Azama (ASFC).

Mataji hayo yalibebwa na warembo watatu, kisha walifuata wachezaji wa Yanga wakiwa wamevalia suti nyeusi na nyuma yao kulikuwa na skauti waliyobeba maputo.

Jambo lililoibua shangwe Uwanja wa Benjamin Mkapa, huku msanii wa bongo fleva, Sir Jay akitumbuiza wimbo uliyojizolea umaarufu wa Ndiyo Huyohuyo.

Wakati huo huo timu ya wanawake ilikuwa inapita pembeni ya majukwaa ya mashabiki ambao walikuwa wanawarushia pesa baada ya kushinda mechi dhidi ya Ilala Queens.

Baada ya wachezaji hao kuzunguka uwanja mzima kisha wakasimama kupiga picha na kuanza kugawa zawadi ya kofia kwa mashabiki wao.