Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Jezi ya Simba yaipiga bao ya Yanga

JEZI za Simba ndizo zimeonekana kuwa nyingi eneo la Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini hapa huku zile za watani wao Yanga zikiwa za kuhesabika.

Leo Jumatatu Agosti 31, 2020 Simba inacheza mechi ya kirafiki na AFC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ambapo nje ya uwanja kuna wafanyabiashara wanauza jezi hizo lakini jezi za Simba pekee ndizo zimetandazwa kwa wingi.

Mmoja wa wafanyabiashara hao Emmanuel Mgonja amesema kuwa mauzo ya jezi za Yanga msimu huu yamekuwa hafifu ndio sababu kubwa ya kushindwa kuendelea kununua jezi hizo.

Amesema kuwa udhibiti wa jezi za Yanga uliofanywa na kampuni inayowadhamini GSM pia imefanya jezi hizo kuadimika viwanjani.

"Huwa nasafiri mikoani kuuza tu jezi pale michezo ya timu  hizi zinapocheza lakini tangu kuanza kwa msimu ulioisha jezi hizo zimekuwa hazilipi, kwani zinatoka moja moja sana, pia GSM wamekuwa wakifanya ukaguzi mno juu ya hizo jezi na ukikamatwa nazo bila kibali ni kesi," amesema Mgonja

Amina Mohamed amesema mauzo ya jezi za Yanga ni madogo kutokana na timu hiyo kutokufanya vizuri msimu uliopita ikiwemo kukosa makombe ya michuano yote.