Dar City wanatupia tu BDL

Muktasari:
- Dar City imefunga pointi hizo, kutokana na michezo nane, ikiongoza pia katika msimamo wa ligi hiyo kwa pointi 16.
Dar City inaongoza kwa kufunga pointi 756, katika Ligi ya Mkoa wa Dar es Salaam (BDL).
Dar City imefunga pointi hizo, kutokana na michezo nane, ikiongoza pia katika msimamo wa ligi hiyo kwa pointi 16.
Inayofuatia ni Savio iliyofunga pointi 654, Stein Warriors 594, JKT 580, KIUT 538, Srelio 523, Kurasini Heat 497, ABC 493 na Vijana ‘City Bulls’ 492.
Nyingine ni Mchenga Stars 485. Pazi 467, UDSM 440, Chui 418, Polisi, 402, na Mgulani JKT 387 .
Kocha wa kikapu wa Dar City, Mohamed Mbwana alisema ligi ya mwaka huu imekuwa na ushindani mkubwa tofauti na miaka ya nyuma.
“Ushindani huu ndiyo unaotakiwa, nachojua kupitia mashindano haya viwango vinaweza vikaongezeka,” alisema Mbwana.