Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Daktari aitungia shairi Taifa Stars

Muktasari:

 

  • Taifa Stars imefuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa mara ya pili baada ya kufanya hivyo mwaka 1980.

Dar es Salaam. Daktari wa Wilaya ya Itilima, Beatus Chikoti ametunga shairi maalum la kuisifia timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' baada ya kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika Misri mwezi Juni.

Stars ilijihakikishia tiketi yake ya AFCON baada ya kuibanjua Uganda kwa mabao 3-0 katika mchezo wa mwisho wa kundi L uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa.

Kutokana na matokeo ya Cape Verde kutoka sare ya bila kufungana, Stars iliungana na Uganda kusonga mbele kwani ilifikisha pointi nane katika mechi zote sita za kundi hilo.

Katika shairi lake, Dokta Chikoti ameifananisha Stars na mdudu Kakakuona ambaye amekuwa haonekani mara kwa mara

KAKAKUONA KONGOLE

1.  Miaka thalatha kenda, mwaka huu imetimia

Tokea uliposhinda, na ukafuzu sawia

Hatimaye ukaenda, nchini Naijeria Kakakuona kongole,

kuweka historia.

2. Miaka arobaini, kimsingi nakwambia

Tino aliposaini, kwenye lango la Zambia

Juzi Msuva na Nyoni, nao wakairudia

Kakakuona kongole, kuweka historia.

3. Agirei wa Morisi, ushindi kapalilia

Kwa uchu mithili fisi, kichwa alipigilia

Tukafurahi na sisi, heshima kujipatia

Kakakuona kongole, kuweka historia.

4. Jella Mtemi na Tenga, ujana wakumbukia

Shindanoni walitinga, nchi wakapigania

Shabaha wakailenga, jambo hilo kurudia

Kakakuona kongole, kuweka historia.

5. Ilibidi kusubiri, kwa miongo tukilia

Tulikosa ujasiri, wengine kuwatambia

Ama tulitahayari, kwa vichapo kuchezea

Kakakuona kongole, kuweka historia.

6. Mbwana Ali Samatta, nahodha alotimia

Beji alipofumbata, moyoni alinuia

Kufuzu tupate pata, na hilo limetimia

Kakakuona kongole, kuweka historia.

7. Ukuta ule imara, hakika umetulia

Mbaga hana masihara, Yondani na Kessy pia

Hawakuwa na papara, ulinzi kusimamia

Kakakuona kongole, kuweka historia.

8. Boko ni mpiganaji, jemedari asilia,

Faridi naye kipaji, Mudathiri ana nia

Manula mtia chaji, na mikwaju kuzuia

Kakakuona kongole, kuweka historia.

9. Fei Toto ni mahiri, pindi anapoingia

Wengine wote hodari, nchi wametumikia

Kapombe aliumia, naye pia askari

Kakakuona kongole, kuweka historia.

10. Amunike namsifu, heshima katuletea

Mkali kama siafu, nidhamu kasimamia

Heko kwa tiefuefu, na ile kamati pia

Kakakuona kongole, kuweka historia.

11. Rais nakupongeza, morali uliwatia

Na sasa umeongeza, viwanja kuwapatia

Hakika inapendeza, kwa sote watanzania

Kakakuona kongole, kuweka historia.

 

12. Kakakuona geuka, na ushindi dumishia

Usije kuadimika, kwa miongo kupotea

Misri kapige soka, tuzo zipate tujia

Kakakuona kongole, kuweka historia.