Kumbe kipa Grimsby imemuuma sana
Muktasari:
- Hata hivyo, kipa huyo amefichua kwamba yeye ni shabiki wa Man United, hivyo alikasirishwa na matokeo hayo, ambapo Grimsby ilishinda kwa kwa mikwaju ya penalti 12-11 baada ya sare ya mabao 2-2 katika muda wa kawaida.
LONDON, ENGLAND: KIPA wa Grimsby Town, Christy Pym amewashangaza mashabiki kwa namna alivyokuwa akishangilia baada ya kuitupa nje Manchester United kwenye Kombe la Ligi, lakini kumbe jambo hilo limemuuma sana.
Hata hivyo, kipa huyo amefichua kwamba yeye ni shabiki wa Man United, hivyo alikasirishwa na matokeo hayo, ambapo Grimsby ilishinda kwa kwa mikwaju ya penalti 12-11 baada ya sare ya mabao 2-2 katika muda wa kawaida.
Pym, 30, ambaye aliokoa hatari kadhaa katika mechi hiyo ikiwamo kwenye tukio la kupigiana penalti, ambapo alidaka mkwaju wa Matheus Cunha.
Licha ya ushindi huo, kipa huyo alisema hakuwa na furaha sana kwa sababu alikuwa kwenye njia panda, Man United ni timu yake anayoshabiki.
Alisema: "Mimi ni shabiki wa Man United, hivyo nimechukia kiasi. Usiku kama huu ndio unaofanya tucheze soka. Ningeweza kufanya vizuri zaidi, sivyo?
"Niliokoa penalti moja ili timu iwepo mchezoni na vijana walifanya walichobaki."
Pym alitua Blundell Park mwezi uliopita baada ya kusaini dili la miaka miwili akiwa mchezaji huru baada ya kuachana na Mansfield Town kwenye dirisha hili.
Kipa huyo aiwahi kuwa kwenye akademia ya Man United na kucheza sambamba na Marcus Rashford na Scott McTominay. Hata hivyo, aliachwa 2019 na kwenda kucheza soka kwenye ligi za chini.
MECHI ZIJAZO ZA KOMBE LA LIGI MSIMU HUU
Port Vale vs Arsenal
Lincoln City vs Chelsea
Tottenham vs Doncaster
Huddersfield vs Man City
Liverpool vs Southampton
Fulham vs Cambridge
Brentford vs Aston Villa
Barnsley vs Brighton
Swansea vs Nottingham Forest
Newcastle United vs Bradford
Sheffield Wednesday vs Grimsby Town
Wolves vs Everton
Crystal Palace vs Millwall
Burnley vs Cardiff City
Wrexham vs Reading
Wigan vs Wycombe Wanderers