VIDEO: Gari la wazi lakwamisha Yanga kutoka

MABINGWA wa Ligi Kuu Bara, Yanga wametua wakitokea Mbeya walikokabidhiwa taji lao la msimu huu saa 5:49 asubuhi na kubaki ndani kwa muda wakisubiri gari ya wazi maalum kwaajili ya kubeba kombe.


🔴#LIVE: SHEREHE za UBINGWA YANGA muda huu....!!!!!! KIMEWAKAAAA


Wametumia dakika 26 kusubiri gari hilo ambalo lilifika saa 12:15 ndipo timu ilipoanza kutoka tayari kwaajili ya kuingia ndani ya gari hiyo.

Mashabiki wachache waliofanikiwa kuingia ndani ya Uwanja walisikika wakisema gari maalum kwaajili ya kubena kombe imefika.

“Hii kiboko sisi ndio Yanga wa kimataifa walijua ni kiki mambo si ndo hayo aya ongeeni wananchi wamefanya yao,” ni maneno ya mashabiki ndani ya Uwanja.



MASTAA WAFUATWA NDANI

Pamoja na mashabiki kukaa kwa muda wakisubiri mastaa wao wakitoka gari iliingiq ndani ya na kufuata mastaa wao.

#LIVE: Mapokezi ya UBINGWA YANGA muda huu....!!!!!!



Kiungo Feisal Salum, Djuma Shabani, Herietie Makambo, Jesus Moloko, Salum Abubakar, Fiston Mayele, Haji Manala na Dikson Job, Kibwana Shomari na David Bryson wamekaa juu ya gari hiyo.