Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Uwayezu Francois CEO mpya Simba SC

Muktasari:

  • Francois, alikuwa Makamu Mwenyekiti wa APR ya Rwanda na amewahi pia kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka cha Rwanda (FERWAFA).

Uongozi wa Simba umemtangaza Uwayezu Francois Regis raia wa Rwanda kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, akichukuwa nafasi ya Imani Kajula anayejiandaa kumaliza mkataba mwishoni mwa mwezi huu.

Francois, alikuwa Makamu Mwenyekiti wa APR ya Rwanda na amewahi pia kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka cha Rwanda (FERWAFA).

Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Simba kuwa na CEO kutoka nje ya nchi, kwani awali iliwahi kumuajiri, Senzo Mbatha kutoka Afrika Kusini ambaye baadaye alijiondoa na kutua Yanga kabla ya kurithiwa na Mzambia, Andre Mtine aliyetokea klabu ya TP Mazembe ya DR Congo.