Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kahama Sixers yaendeleza moto

KAHAMA Pict

Muktasari:

  • Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana fainali  ya  mwaka jana,  Kahama iliishinda Risasi  michezo 3-1.

KLABU ya Kikapu ya Kahama Sixers imeanza vizuri kampeni ya kutetea taji la ubingwa wa Ligi ya Mkoa wa Shinyanga, baada ya kuifunga Risasi kwa pointi 54-46, katika mchezo uliopigwa  kwenye Uuwanja wa Kahama, mjini humo.

Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana fainali  ya  mwaka jana,  Kahama iliishinda Risasi  michezo 3-1.

 Kahama Sixers ilianza mchezo kwa robo ya kwanza kwa kasi, hali iliyofanya  iongoze  kwa pointi 19-11, robo ya pili, Risasi iliongoza kwa  pointi 16-8.

Robo ya tatu ilipoanza mchezo ulizidi kuwa mkali na kila timu kuongeza kasi na kuwa mchezo wa funga nikufunge, hadi robo hiyo  inamalizika zilikuwa  zimefungana pointi 11-11 na robo ya nne Kahama ikapata  pointi 16-8.

Kwa ufungaji, Vicent Mangula  wa  Risasi,  alitupia pointi 16  akifuatiwa na Hemed Magoti aliyefunga 13.

B4 Mwadui, Risasi, Kahama Sixers na Veta ndizo zinazoshiriki na Kamishina wa Ufundi na Mashindano wa Ligi ya Kikapu Shinyanga, George Simba, alisema mfumo wa ligi hiyo, kila timu itacheza nyumbani na ugenini ili kuja kupata bingwa wa msimu huu.