Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Jabir afunguka baada ya kutua Ubelgiji

Baada  ya kutua katika klabu ya KAA Gent ya nchini Ubelgiji kwa majaribio ,Anuary Jabir amesema atapambana kufanikisha  ndoto yake ya muda mrefu ya kucheza soka la kulipwa.

Jabir ambaye anaichezea Kagera Sugar aliondoka juzi nchini kwenda Ubelgiji kwa ajili ya kufanya majaribio katika klabu hiyo inayoshiriki ligi daraja la kwanza.

Akizungumza na Mwanaspoti kutokea nchini Ubelgiji, Jabir alisema amefurahi kupata nafasi hiyo na atapambana kuhakikisha ndoto yake hiyo inatimia.

Mshambuliaji huyo  huyo ambaye amewahi kuwa mfungaji bora wa ligi daraja la kwanza msimu wa 2019-2020 wakati huo akichezea Dodoma Jiji alisema amepokelewa vizuri na wenyeji wake na  anaamini atafanya vizuri katika majaribio hayo.

Straika huyo mpaka anaondoka nchini alikuwa ameifungia Kagera Sugar mabao matano kwenye Ligi Kuu Bara na amewahi kuwa mchezaji bora wa ligi kuu kwa mwezi Februari mwaka 2021.