Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Fountain Gate hesabu zipo kwa Wagosi

GATE Pict

Muktasari:

  • Fountain ipo nafasi ya 14 juu ya timu mbili zilizoshuka daraja mapema KenGold na Kagera Sugar na inapambana kuepuka kucheza play-off ya kushuka daraja inayosubiriwa kufahamika baada ya mechi za Juni 22 ili kupata nafasi ya kuvaana na Stand United inayosaka kupanda Ligi Kuu.

NI kufa au kupona. Ndivyo unavyoweza kusema wakati Fountain Gate itakapokuwa ugenini kukabiliana na Coastal Union, Juni 18 katika mechi ya Ligi Kuu Bara ikiwa inahitaji ushindi wa ina yoyote ili kuepuka janga la kucheza play-off ya kushuka daraja.

Fountain ipo nafasi ya 14 juu ya timu mbili zilizoshuka daraja mapema KenGold na Kagera Sugar na inapambana kuepuka kucheza play-off ya kushuka daraja inayosubiriwa kufahamika baada ya mechi za Juni 22 ili kupata nafasi ya kuvaana na Stand United inayosaka kupanda Ligi Kuu.

Kocha wa Fountain Gate, Amri Said  ‘Stam’ alisema wapo nafasi mbaya wanapambana kujiweka tayari kuhakikishi mechi dhidi ya Coastal Union wanahakikisha wanapata pointi tatu muhimu kuwarudisha kwenye ushindani lakini pia kujihakikishia nafasi ya kusalia moja kwa moja.

“Tuna dakika 90 ngumu ugenini dhidi ya Coastal matokeo tutakayoyapata dhidi yao ndiyo yataamua hatma yetu kukwepa mtego wa kucheza prayoff na hilo linawezekana kama mikakati yetu itaenda kama tulivyopanga,” alisema Stam na kuongeza;

“Tunatambua umuhimu wa mechi zote mbili zilizobaki lakini tunaamini matokeo ya ushindi mbele ya Coastal Union yataturudisha mchezoni na kutupa uhakika wa kucheza ligi msimu ujao.”

Akizungumzia wapinzani wao alisema na wao wanazihitaji pointi hizo muhimu lakini dakika 90 ndio zitakazoamua ubora huku akiutaja ukuta wake kuwa umeimarika na hautakuwa sehemu ya wao kudondosha pointi hizo tatu.

Said alisema ni kweli hawapo vizuri kwenye safu yao ya ulinzi kutokana na kuwa timu ambayo imekuwa ikiruhusu mabao amefanyia marekebisho kwa kuwajenga wachezaji wao kupunguza makosa madogo madogo.

“Ni kweli hatuna safu nzuri ya ulinzi kutokana na makosa madogo madogo waliyokuwa nayo kwa kuruhusu mabao mengi zaidi msimu huu siwezi kuzungumza kwa kuaminisha umma tumefanya maboresho, sio kweli kwa sababu dirisha bado kilichofanyika ni kusawazisha makosa.”