Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wasanii  kupima afya bure

Nyerere 01
Nyerere 01

Muktasari:

  • Akizungumza jijini Dar es Salaam leo,  Dk Peter Kisenge amesema, tukio hilo linaanza mwezi huu wa Desemba 2024 hadi Januari mwakani, kila wikiendi kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni katika Kliniki ya JKCI Kawe iliyopo Kawe jengo la Mkapa Health Plaza barabara ya Tuari jijini.

Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), iliyoko Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, imetangaza huduma ya kupima moyo bure kwa wasanii wa filamu nchini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo,  Dk Peter Kisenge amesema, tukio hilo linaanza mwezi huu wa Desemba 2024 hadi Januari mwakani, kila wikiendi kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni katika Kliniki ya JKCI Kawe iliyopo Kawe jengo la Mkapa Health Plaza barabara ya Tuari jijini.

 Kisege amesema,  wameamua kutoa huduma hiyo kwa nia ya kuokoa wasanii wengi wanaopata maradhi ya moyo na kukosa matibabu ya haraka.

Nyerere 02

"Taasisi ya Moyo tumeamua kushirikiana na nyie wasanii wote ili kuweza kuwasaidia kujikinga na magonjwa yasiyoambukizwa, na tumeamua kufanya zoezi hili la kupima katika kliniki yetu ya Kawe kila Jumamosi na Jumapili ambapo tutatoa matibabu bure sababu afya ndio kitu cha msingi, hatutaki kusikia labda msanii ameanguka akiimba, au  ameanguka akiwaaigiza  sababu tukigundua," amesema Daktari huyo aliyeongeza;

Nyerere 03

 "Na kwa kuwa wasanii ni kioo  cha jamii, basi watatusaidia sana kuwaeleza wengine  jinsi ya kujikinga na haya magonjwa yanayochangia vifo, duniani kote, magonjwa yasiyoambukiza  yanaua  watu karibia milioni 17 kwa hapa nchini ,  yanachangia asilimia 9 na serikali inatumia hela nyingi sana sababu watu wengi hawajui  wana shinikizo la damu."

Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steve Nyerere, amezungumza kama Mwakilishi wa Wasanii na kuushukuru uongozi wa Muhimbili pamoja na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa kujua umuhimu wa Wasanii wa Filamu na kuamua kuwashika Mikono katika natibabu ya maradhi ya moyo.

"Ni jambo jema Dokta Kisenge anaungana na wasanii,  na amekuja  kuiokoa kiwanda cha filamu chote bila kujali huyu msanii mchanga au mkongwe, hii kauli ya kusema kupima bure ni haina siasa bali ameangalia afya kwanza  ambayo inayoleta amani katika taifa letu.

"Ametupa muelekeo wa tasnia ya maisha  tunavyotakiwa kuishi, nasi watanzania tunapenda neno bure, hivyo niwaombe wasanii wenzangu  tujitokeze kwa wingi tukapime  leo hii  kujigundua afya utaishi kwa umakini na tahadhari,  kama hujapima kila kitu utakachokifanya utaona ni sahihi kwako kwani hujui afya yako" amesema Steve Nyerere.