Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Pastor Myamba kumbe alikuwa hatanii

Muktasari:

Pastor Myamba anamiliki kanisa hilo eneo la Kigamboni, ikiwa ni muda mrefu tangu amiliki chuo cha uigizaji kilichosaidia kuibua vipaji vipya vya sanaa nchini.

KUMBE ile staili yake ya kuigiza ya kichungaji katika filamu alizocheza mwigizaji nyota nchini, Emmanuel Myamba ‘Pastor Myamba’ haikuwa utani, kwani jamaa kwa sasa anamiliki kanisa lake.

Pastor Myamba anamiliki kanisa hilo eneo la Kigamboni, ikiwa ni muda mrefu tangu amiliki chuo cha uigizaji kilichosaidia kuibua vipaji vipya vya sanaa nchini.

“Naamini kuigiza ni sehemu ya kuhubiria maana filamu ni njia ya kufikisha ujumbe kwa hadhira, hivyo ninaigiza, pia ni natoa huduma ya kiroho katika kanisa la The World Life Ministry kama mchungaji,” alisema .

Msanii huyo ni mmoja wa waigizaji waliobobea kuigiza kama mchungaji katika filamu za kidini tangu enzi za marehemu Steven Kanumba, kiasi cha baadhi ya mashabiki wake kumtabiria kuja kuwa kiongozi wa kiroho, jambo lililokuwa kweli kwa sasa.