Tamu, chungu uteuzi wa Taifa Stars

Muktasari:

Wakati wachezaji 23 wakifurahia kuandika historia ya kushiriki fainali hizo kwa mara ya pili, hali inaweza kuwa ngumu kwa nyota tisa ambao watalazimika kurejea nyumbani na kuyashuhudia mashindano hayo kupitia luninga.

Dar es Salaam. Ni fursa na heshima kwa mchezaji kuitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa kinachoshiriki mashindano ya kimataifa kama vile Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON), lakini mambo hugeuka pindi anapokosa nafasi hiyo dakika za lala salama.

Ndivyo hali inavyoweza kuwa kwa nyota 23 walioteuliwa na benchi la ufundi kuunda kikosi cha Taifa Stars kitakachoshiriki AFCON, wakitokea katika orodha ya wachezaji 32 waliokuwemo katika timu ya awali kujiandaa na fainali hizo.

Wakati wachezaji 23 wakifurahia kuandika historia ya kushiriki fainali hizo kwa mara ya pili, hali inaweza kuwa ngumu kwa nyota tisa ambao watalazimika kurejea nyumbani na kuyashuhudia mashindano hayo kupitia luninga.

Wachezaji tisa watakaokosa AFCON baada ya kushindwa kupenya katika kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 ni makipa Selemani Salula na Claryo Boniface, mabeki Abdi Banda na David Mwantika, viungo Fred Tangalu, Miraji Athumani na Shiza Kichuya na kinda Kelvin John ‘Mbappe’.

Kutemwa kwa wachezaji hao na uteuzi wa wenzao 23 haukutokea kwa bahati mbaya, bali ni matokeo ya tathmini ya kina iliyofanywa na Kocha Emmanuel Amunike katika kipindi chote kabla na wakati wa maandalizi ya timu hiyo kabla ya fainali hizo.

Banda anayecheza nafasi ya beki katika klabu ya Baroka ya Afrika Kusini huenda akawa ametibuliwa na ukosefu wa ufiti wa mechi jambo ambalo limechangiwa kwa kiasi kikubwa kutopata nafasi ya kutosha katika idadi kubwa ya mechi za timu yake huko Afrika Kusini.

Majeraha hayo yalichangia kumuweka nje Banda kwenye idadi kubwa ya mechi hasa za mzunguko wa pili na hata alipopona aliendelea kusugua benchi katika kikosi ambacho msimu uliopita alicheza mechi 15 tu za Ligi Kuu Afrika Kusini.

Pia haishangazi kuachwa mshambuliaji Shabani Chilunda ambaye hivi karibuni amevunja mkataba wake na CD Tenerife ambayo ilimtoa kwa mkopo CD Izarra inayoshiriki Ligi Daraja la Tatu Hispania.

Chilunda amepita kipindi kigumu Hispania kutokana na kutopata nafasi ya kucheza na kwa kudhihirisha hilo, katika msimu mzima amecheza michezo 10 tu ambapo mitatu akiwa na Tenerife tena akicheza dakika 28,