Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Usyk, Dubois kumaliza ubishi Wembley

MASUMBWI Pict

Muktasari:

  •  Hili siyo pambano la kawaida, bali ni fursa ya kihistoria kwa mmoja wao kuandika upya jina lake katika orodha ya mabondia wakubwa zaidi wa wakati wote.

SIKU zinawadia. Uwanja wa Wembley, jijini London, unatarajiwa kuwa kitovu cha dunia ya ngumi Julai 19, 2025, wakati mabondia wakubwa Oleksandr Usyk na Daniel Dubois watakapoingia ulingoni kwa pambano la marudiano la ubingwa wa dunia wa uzito wa juu.

 Hili siyo pambano la kawaida, bali ni fursa ya kihistoria kwa mmoja wao kuandika upya jina lake katika orodha ya mabondia wakubwa zaidi wa wakati wote.

Oleksandr Usyk, ambaye ni raia wa Ukraine, ana rekodi ya kushinda mapambano yote 23 aliyopigana na 14 kati ya hayo alishinda kwa KO.

Amekuwa bingwa wa dunia katika uzito wa kati (cruiserweight) na baadaye katika uzito wa juu, na anarejea Wembley akiwa bingwa wa mikanda ya WBA, WBO na WBC baada ya kumshinda Tyson Fury katika pambano la kusisimua  Mei 2024.

Kwa upande mwingine, Dubois, ambaye ni raia wa  Uingereza mwenye rekodi ya kushinda mapambano 22  na kupoteza mawili, amekuwa akipanda chati kwa kasi.

 Mwaka 2023 alipoteza mbele ya Usyk kwa TKO katika raundi ya tisa. Baada ya hapo, Dubois alirudi kwa kishindo kwa kumshinda Anthony Joshua na kunyakua taji la IBF lililokuwa na sasa ana nafasi ya kulipa kisasi mbele kwa Usyk.

Mbali ya pambano hili ambalo litahudhuriwa na mashabiki takribani 90,000, pia kutakuwa na mapambano ya utangulizi mawili ambayo ni  ubingwa wa dunia wa uzito wa cruiser lile la Lawrence Okolie dhidi ya Kevin Lerena.

Pia kutakuwa na pambano la uzito wa juu la England kati ya Viktor Vykhryst na Frazer Clarke.

Matangazo ya pambano hili yanatarajiwa kuanza saa 6:45 usiku kwa saa Afrika ya Mashariki.

Wataalamu wengi wa mchezo huu wanampa nafasi Usyk kutokana na uzoefu na historia yake ya kutopigwa, lakini wengine wanaamini Dubois anaweza kuleta mshangao, hasa kwa nguvu na hasira aliyonayo juu ya kutaka kulipa kisasi.

 Derek Chisora, ambaye ni bondia mkongwe wa Uingereza, alisema: “Dubois anahitaji kuwa pepo kichaa (crazy demon) ili kumshinda Usyk.”