Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

UEFA ni Waingereza, Wahispania nusu fainali

Timu nne za Hispania na England zitakutana katika mechi za nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa wa soka barani Ulaya baada ya Manchester City na Liverpool kulazimisha sare dhidi ya Atletico Madrid na Benfica katika mechi za nusu fainali jana (Jumatano).


Manchester City itakutana na Real Madrid katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa wa soka barani Ulaya baada ya kuiondoa Atletico Madrid jana kwa jumla ya bao 1-0, wakati vigogo wengine wa England, Liverpool watakutana na Villareal.


Bao la Kevin De Bruyne alilofunga wiki iliyopita katika mechi ya kwanza ya robo fainali kwenye uwanja wa Etihad lilitosha kuivusha timu ya Pep Guardiola baada ya mechi ya marudiano iliyofanyika jana nchini Hispania kushindwa kuzalisha goli lolote.
Manchester City imefika nusu fainali kwa mwaka wa pili mfululizo.