Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Rani Khedira kuitumikia Tunisia Kombe la Dunia 2026

RANI Pict

Muktasari:

  • Hatua hiyo inamruhusu Khedira kuichezea Tunisia, ambayo itashiriki mashindano ya Kombe la Dunia 2026 yatakayofanyika kwa ushirikiano wa Marekani, Mexico na Canada kuanzia Juni 11, 2026 na yatamalizika Julai 19, 2026.

KIUNGO wa Union Berlin ya Ujerumani, Rani Khedira, amethibitishwa rasmi kuitumikia timu ya taifa ya Tunisia, baada ya kupewa kibali cha mwisho na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) sambamba na Shirikisho la Soka Afrika (CAF). 

Hatua hiyo inamruhusu Khedira kuichezea Tunisia, ambayo itashiriki mashindano ya Kombe la Dunia 2026 yatakayofanyika kwa ushirikiano wa Marekani, Mexico na Canada kuanzia Juni 11, 2026 na yatamalizika Julai 19, 2026.

Shirikisho la Soka la Tunisia (FTF), limetangaza kwamba jopo la haki la FIFA limeidhinisha uraia wa kimichezo wa Khedira, na kumfanya kuwa sehemu ya kikosi cha The Carthage Eagles. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 anatabiriwa kuwa msaada mkubwa katika safu ya kiungo, akitarajiwa kuleta uzoefu na nguvu ya kiufundi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Khedira kukubali kuwakilisha Tunisia, licha ya hapo awali kukataa wito huo mwaka 2018. Khedira alizaliwa Stuttgart na kucheza kwa ngazi ya timu za taifa za vijana za Ujerumani, lakini ana sifa za kimichezo za kuichezea Tunisia kupitia baba yake.

Uamuzi huu unakamilisha jitihada za muda mrefu za Tunisia za kumshawishi Khedira kujiunga na timu yao ya taifa, na kuonyesha matumaini makubwa kwa mashindano ya kimataifa yajayo.

Huyu ni mdogo wa kiungo wa zamani wa Real Madrid, Juventus, VfB Stuttgart na Hertha BSC, Sami Khedira ambaye alikuwepo katika kikosi cha Ujerumani kilichoshinda Kombe la Dunia 2014.