Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Nani abaki, aondoke Arsenal

Arsenal Pict

Muktasari:

  • Kwenye dirisha la mwisho la majira ya kiangazi katika zama za Edu, Arsenal ilifanya usajili wa mastaa watatu tu - ikiwamo uhamisho wa jumla wa kipa David Raya, ambaye mwanzoni alikuwa kwenye kikosi chao kwa mkopo, huku usajili mwingine wa wachezaji wawili waliofanya katika dirisha hilo la mwaka jana, iliwanasa kwa mkopo.

LONDON, ENGLAND: BAADA ya kushuhudia majeruhi wakitibua mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu, Arsenal inaweza kuchukua uamuzi wa kupangua kikosi kwa kuondoa baadhi ya mastaa na kuleta wengine wapya kwenye dirisha lijalo la majira ya kiangazi.

Kwenye dirisha la mwisho la majira ya kiangazi katika zama za Edu, Arsenal ilifanya usajili wa mastaa watatu tu - ikiwamo uhamisho wa jumla wa kipa David Raya, ambaye mwanzoni alikuwa kwenye kikosi chao kwa mkopo, huku usajili mwingine wa wachezaji wawili waliofanya katika dirisha hilo la mwaka jana, iliwanasa kwa mkopo.

Lakini, iliingiza zaidi ya Pauni 70 milioni pamoja na nyongeza nyingine za bonasi kwa kuwauza mastaa wake iliyowatoa kwenye akademia ambao ni Eddie Nketiah na Emile Smith Rowe, ikiwa ni miongoni mwa iliyowauza.

Sasa mrithi wa Edu, atakuwa na kibarua kizito cha kufanya usajili dirisha lijalo la majira ya kiangazi na kwa sasa inaelezwa, Andrea Berta ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kwenda kuongoza idara hiyo ya kuuza na kununua mastaa Emirates.

Kama atateuliwa mwezi huu, basi atakuwa na muda mchache wa kujiandaa kuanza kufikiria ni mchezaji gani wa kuja kuongeza nguvu kwenye kikosi ili kiwe cha kiushindani msimu ujao.

Kutokana na mtangulizi wake, Edu kupata sifa kubwa kwa aina ya wachezaji aliowasajili na wale aliowaondoa kuifanya timu hiyo kuwa na nguvu na kushindania mataji, mrithi huyo atakuwa na kazi kubwa ya kuamua nani atoke na nani abaki kabla ya kuingia sokoni kusajili mchezaji mpya. Kuna wachezaji kibao wanahusishwa na Arsenal, wakiwamo mastraika, ambao wamekuwa wakitajwa mara kwa mara kama vile Benjamin Sesko na Alexander Isak.

Lakini, kwa sasa kitu kinachotazamwa ni wachezaji waliopo wanaounda kikosi cha Arsenal, je ni nani anapaswa kubaki na yupi wa kufunguliwa mlango wa kutokea kwenye dirisha lijalo la usajili? Kocha Arteta anataka kuwa na timu itakayokuwa na uwezo wa kushinda ubingwa wa Ligi Kuu England msimu ujao endapo kama itashindikana msimu huu.


David Raya - ABAKI

Neto - AONDOKE

Karl Hein - AONDOKE

William Saliba - ABAKI

Ben White - ABAKI

Gabriel - ABAKI

Jurrien Timber -  ABAKI

Jakub Kiwior - ONDOKE

Oleksandr Zinchenko - AONDOKE

Takehiro Tomiyasu - ABAKI

Riccardo Calafiori - ABAKI

Myles Lewis-Skelly - ABAKI

Nuno Tavares - AONDOKE

Thomas Partey - AONDOKE

Martin Odegaard -  ABAKI

Jorginho - AONDOKE

Mikel Merino - ABAKI

Declan Rice - ABAKI

Albert Sambi Lokonga - AONDOKE

Fabio Vieira -  AONDOKE

Ethan Nwaneri - ABAKI

Reiss Nelson - AONDOKE

Marquinhos - AONDOKE

Kai Havertz - ABAKI

Bukayo Saka - ABAKI

Gabriel Jesus - ABAKI

Gabriel Martinelli - ABAKI

Leandro Trossard - ABAKI

Raheem Sterling - AONDOKE