Klopp:Tumecheza chini ya kiwango
Muktasari:
- KOCHA wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema vijana wake walionyesha kiwango dhaifu kwenye mchezo wao wa robo fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid jambo lililopeleka kupata kipigo cha mabao 3-1.
MADRID, HISPANIA. KOCHA wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema vijana wake walionyesha kiwango dhaifu kwenye mchezo wao wa robo fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid jambo lililopeleka kupata kipigo cha mabao 3-1.
Mjerumani huyo alisema, "Ikiwa unahitaji kwenda hatua ya nusu fainali kuna jambo muhimu ambalo unapaswa kufanya, lakini sisi hatukulifanya usiku wa leo (jana). Hatukucheza soka safi kiasi cha kuifanya Real Madrid kutushambulia.
Katika mchezo huo uliofanyika kwenye uwanja wa Alfredo Di Stefano mchezaji wa Real Madrid,Vinicius Junior alionekana kuwa mwiba mkali kwa Liverpool.
Vinicius alitupia mabao mawili na Marco Asensio akitupia moja huku bao la kufutia machozi la Liverpool likifungwa na Mohamed Salah.
Liverpool ina mlima mrefu wa kupanda katika mchezo wa marudiano utakaofanyika Anfield Aprili 14 wakitakiwa kupata ushindi wa mabao 2-0 au zaidi ili kutinga hatua ya nusu fainali.
Wakati Liverpool ikikumbana na kipigo hicho cha mabao 3-1 wakiwa ugenini, Manchester City ilianza vizuri robo fainali ya kwanza kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Borussia Dortmund ya Ujerumani ,mabao ya washindi yalifungwa na Kevin De Bruyne na Phil Foden