Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Enzo Maresca: Ninajivunia kuwa kocha wa Estevao Willian

ENZO Pict

Muktasari:

  • Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18, aligeuka kuwa mfungaji mdogo zaidi wa Chelsea katika Ligi ya Mabingwa, alipofunga penalti kwa utulivu mkubwa na kuifanya Chelsea iwe mbele kwa 4-1 hadi mapumziko. Akiwa katika kiwango cha juu, Estevão aliwasumbua mabingwa wa Ulaya mara nne na kuongeza matarajio makubwa tangu afike London Magharibi.

Kocha wa Chelsea, Enzo Maresca amesema ana bahati kubwa kuwa kocha wa kijana mwenye kipaji Estevão Willian, baada ya chipukizi huyo kuonyesha kiwango bora zaidi tangu ajiunge na The Blues katika ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Ajax iliyokuwa na wachezaji 10, kwenye Uwanja wa Stamford Bridge usiku wa Oktoba 22, 2025.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18, aligeuka kuwa mfungaji mdogo zaidi wa Chelsea katika Ligi ya Mabingwa, alipofunga penalti kwa utulivu mkubwa na kuifanya Chelsea iwe mbele kwa 4-1 hadi mapumziko. Akiwa katika kiwango cha juu, Estevão aliwasumbua mabingwa wa Ulaya mara nne na kuongeza matarajio makubwa tangu afike London Magharibi.

Alikuwa mmoja wa vijana watatu waliofunga kwa upande wa Chelsea, Marc Guiu alianza kufunga bao la kwanza la msimu, huku Tyrique George akihitimisha kwa bao la tano, wakati kijana mwenye umri wa miaka 17, Reggie Walsh, akipewa dakika 25 na kuwa mchezaji mdogo zaidi katika historia ya klabu hiyo kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa.

“Najivunia sana,” amesema Maresca, ambaye alifanya mabadiliko 10 katika kikosi chake kwenye mechi ya pili kati ya sita ndani ya siku 21.

ENZ 01

“Ulikuwa usiku maalum kwa klabu na wachezaji wangu vijana. Hii ndiyo mkakati wa klabu, tuna wachezaji wengi vijana. Tulikuwa na timu yenye vijana wa umri mdogo zaidi kwenye Ligi Kuu msimu uliopita, na mwaka huu ni hivyo hivyo.

“Tulibadilisha wachezaji 10, si rahisi kufanya hivyo, lakini tulihitaji kufanya hivyo ili kuepuka wachezaji kuchoka. Kwa wachezaji vijana mara nyingi huwa na wasiwasi.

“Wanacheza mechi moja au mbili, wakifunga, wanaanza kufikiri tayari ni wachezaji wakubwa. Lakini jambo zuri kuhusu Estevão ni kwamba hatuhitaji kuwa na wasiwasi kuhusu hilo.

“Yeye ni mnyenyekevu sana, ana nidhamu, anapenda kufanya kazi kwa bidii. Ana familia bora sana inayomsaidia kwa karibu. Ni mchezaji maalum, lakini hatuhitaji kuwa na hofu kwamba ataanza kujiona. Ni kijana rahisi kabisa.

“Najihisi mwenye bahati kubwa kuwa kocha wake. Mashabiki wanalipa tiketi kuwaona wachezaji kama Cole (Palmer) na Estevão.”