Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Bondia Tyson Fury kuzichapa na Wach

FURRY Pict

Muktasari:

  • Pambano hilo limepangwa kufanyika Julai 24 katika ukumbi wa Max Muay Thai, mjini Pattaya, na linatarajiwa kuonyeshwa mubashara duniani kote kupitia Netflix.

LONDON, ENGLAND: BONDIA Tyson Fury amethibitisha  atarejea ulingoni baadaye mwezi huu kwa pambano moja la mwisho la maandalizi kabla ya kukutana na Anthony Joshua, ambapo atapambana na bondia wa uzito wa juu kutoka Poland, Mariusz Wach, nchini Thailand.

Pambano hilo limepangwa kufanyika Julai 24 katika ukumbi wa Max Muay Thai, mjini Pattaya, na linatarajiwa kuonyeshwa mubashara duniani kote kupitia Netflix.

Mapambano ya kurejea kwa Fury yatafanyika siku moja kabla ya Anthony Joshua kupambana na bondia wa Albania, Kristian Prenga, nchini Saudi Arabia.

FUR 01

Wawili hao wanatarajiwa kushinda mapambano yao bila matatizo makubwa kabla ya kukutana katika pambano kubwa la uzito wa juu la Waingereza wawili baadaye mwaka huu.

Pambano lililosubiriwa kwa muda mrefu kati ya Fury na Joshua lilipiga hatua kubwa baada ya mabondia hao kufikia makubaliano ya awali mapema mwaka huu, jambo lililoweka msingi wa moja ya mapambano makubwa zaidi katika historia ya ngumi za Uingereza.

Hata hivyo, kabla ya pambano hilo la kihistoria, kila mmoja atalazimika kwanza kupita katika pambano lake la mwisho la maandalizi.

Mpinzani wa Fury, Mariusz Wach, ana uzoefu mkubwa zaidi wa ngumi za kiwango cha juu kuliko mpinzani wa Joshua.

Mwaka 2012, Wach alipambana na Wladimir Klitschko kuwania ubingwa wa dunia wa uzito wa juu uliounganishwa, na alimlazimisha bingwa huyo wa Ukraine kupigana raundi zote 12 kabla ya kupoteza pambano lake la kwanza katika maisha yake ya kulipwa.

FUR 02

Hata hivyo, mambo yamebadilika sana tangu wakati huo.

Sasa akiwa na umri wa miaka 46, Wach ana rekodi ya mapambano 39 ya ushindi na 13 ya kushindwa, baada ya kupitia kipindi kigumu katika miaka ya mwisho ya taaluma yake.

Amewahi kushindwa kwa pointi na Dillian Whyte, Hughie Fury na Frazer Clarke, huku chipukizi anayetarajiwa kung'ara, Moses Itauma, akimshinda kwa mtoano ndani ya raundi mbili mwaka 2024.

Kutokana na hali hiyo, macho mengi yataelekezwa si tu kuona kama Tyson Fury atashinda, bali pia jinsi atakavyomudu kumshinda mpinzani ambaye sasa amekuwa kipimo cha uwezo kwa mabondia chipukizi wa uzito wa juu kutoka Uingereza.

Bingwa huyo wa zamani wa dunia ametumia sehemu kubwa ya maandalizi yake nchini Thailand, hivyo kufanya Pattaya kuwa sehemu inayofaa kwa pambano hilo. Baada ya hapo, anatarajiwa kusafiri moja kwa moja kwenda Jeddah, Saudi Arabia, kushuhudia pambano la Anthony Joshua akiwa pembeni ya ulingo kabla ya maandalizi ya pambano lao kuanza rasmi.

FUR 03

Pambano la Julai litakuwa la pili kwa Fury tangu alipomaliza kustaafu kwa muda wa miezi 16. Alirejea mwezi Aprili kwa ushindi wa pointi dhidi ya Arslanbek Makhmudov katika Uwanja wa Tottenham Hotspur, ikiwa ni mara yake ya kwanza kupigana nchini Uingereza baada ya zaidi ya miaka mitatu.

Queensberry Promotions pia imethibitisha kuwa mapato yote yatokanayo na mauzo ya tiketi yatatolewa kwa mashirika ya misaada ya nchini Thailand, huku Fury akitarajiwa kukabidhiwa tuzo ya kwanza kabisa ya WBC Humanitarian kutokana na mchango wake wa kibinadamu.

Akizungumza baada ya kuthibitisha pambano hilo, Fury amesema anafurahia kupigana nchini Thailand, nchi ambayo imekuwa sehemu muhimu ya maandalizi yake ya mapambano.