Bakayoko kulikosa bata la China na Shangai

Muktasari:

Chelsea ilimsajili Bakayoko hivi karibuni kwa usajiliwa Pauni 39.7 milioni, huku ikitoa taarifa kuwa mchezaji huyo anakabiliwa na matatizo ya goti na hali yake haijatengemaa.

London, England. Klabu ya Chelsea imemuacha mchezaji wake mpya Tiemoue Bakayako (22) kwenye orodha ya wachezaji watakaosafiri kwenda China na Singapore kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.

Chelsea ilimsajili Bakayoko hivi karibuni kwa usajiliwa Pauni 39.7 milioni, huku ikitoa taarifa kuwa mchezaji huyo anakabiliwa na matatizo ya goti na hali yake haijatengemaa.

Mchezaji huyo wa zamani wa Monaco alishauriwa na madaktari wa The Blues kuwa hataweza kujiunga na wenzake kwenye safari hiyo.