Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Baada ya kuangusha pointi, Arteta atoa neno zito

ARTETA Pict

Muktasari:

  • Kocha wa Villa, Unai Emery, ameipa timu yake uhai mpya baada ya kuanza msimu kwa kusuasua na kuwa katika hatari ya kushuka daraja, lakini sasa wameshinda mechi 9 kati ya 10 zilizopita.

LONDON, ENGLAND: Mikel Arteta amesisitiza kuwa vinara wa Ligi ya Premia, Arsenal, watarejea wakiwa bora zaidi baada ya fadhaa ya kipigo cha kustua cha 2-1 walichopata kutoka kwa Aston Villa, kilichofungua upya mbio za ubingwa Jumamosi.

Emiliano Buendia alifunga bao la ushindi kwa mkwaju wa mwisho kabisa wa mchezo mkali uliovunja rekodi ya Arsenal ya kutofungwa katika mechi 18 mfululizo.

Leandro Trossard wa Arsenal alitoka benchi na kusawazisha kipindi cha pili baada ya Matty Cash kufungua mabao kwa Villa katika kipindi cha kwanza.

Hilo lilikuwa pambano la kwanza Arsenal kupoteza tangu walipofungwa na Liverpool mwezi Agosti, na ni la pili tu msimu mzima.

ART 01

Kipigo hicho kiliifanya Villa kusogea ndani ya pointi tatu kutoka kileleni, huku Manchester City wakipunguza pengo hadi pointi mbili baada ya ushindi wao dhidi ya Sunderland baadaye Jumamosi.

Arsenal wana historia ya kuporomoka mara tu wanapojijenga kama wapinzani wakuu kwenye mbio za ubingwa.

Wamekuwa washindi wa pili kwa misimu mitatu mfululizo na hawajawahi kutwaa taji tangu 2004.

Lakini Arteta anaamini timu yake itaweza kustahimili presha inayoongezeka.

“Hii ndiyo ligi. Unaenda Old Trafford, St James’ Park, Chelsea, unakuja hapa. Tumekuwa katika viwanja vingi vigumu,” amesema.

“Matokeo yangeweza kuwa tofauti, lakini uhalisia ndiyo huo. Tumekaa mechi 18 bila kupoteza na bado tuko karibu na vinara.”

Amesema sasa ni wakati wa kurejea katika kiwango chao na kuendelea kupambana.

ART 02

Arsenal walipata pigo zaidi pale Arteta alipofichua kuwa jeraha la kifundo cha mguu la beki Cristhian Mosquera ni baya kuliko ilivyodhaniwa.

“Atakuwa nje kwa wiki kadhaa,” amesema.

“Ni zaidi ya tulivyotarajia.”

Kocha wa Villa, Unai Emery, ameipa timu yake uhai mpya baada ya kuanza msimu kwa kusuasua na kuwa katika hatari ya kushuka daraja, lakini sasa wameshinda mechi 9 kati ya 10 zilizopita.

Hata hivyo, Emery hataki kujihusisha na mazungumzo ya ubingwa.

“Sifikirii kuhusu taji. Mchezo wa 38 ni mrefu sana. Sisi si wagombea,” amesema.