Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

ATM YA WIKI: Suarez anastaafu Uruguay na maokoto

Muktasari:

  • Suarez mwenye umri wa miaka 37 mbali ya kustaafu timu ya taifa pia haonekani kuwa mbali sana kustaafu upande wa klabu pia kutokana na umri wake.

FLORIDA, MAREKANI: WIKI iliyopita moja kati ya stori kubwa ilikuwa ni Luis Suarez kustaafu timu ya  taifa ya Uruguay aliyoanza kuichezea tangu mwaka 2007.

Suarez mwenye umri wa miaka 37 mbali ya kustaafu timu ya taifa pia haonekani kuwa mbali sana kustaafu upande wa klabu pia kutokana na umri wake.

Lakinu hata kama akistaafu staa huyu ana utajiri wa kutosha utakaomfanya aendelee kuishi kishua bila ya shida yoyote.

Leo tumekusogezea hapa jinsi anavyopata pesa na utajiri alionao hadi sasa.

ANAPIGAJE PESA

Kwa sasa staa huyu anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia Dola 70 milioni ambayo ni mjumuisho wa madili yake ya nje ya uwanja na mishahara aliyokusanya kuanzia mwanzo wa maisha yake ya soka hadi ssa.

Kwa sasa staa huyu anapokea mshahara unaofikia Dola 1 milioni kwa mwaka hiyo ikiwa ni mjumuosho wa bonasi mbalimbali.

Alikubali kuchukua kiasi hicho na kuacha karibia Dola 200,000 kwa mwezi aliyokuwa anaipata Gremio ili aungane na rafiki yake Lionel Messi.

Mbali ya mshahara wake Suarez amekunja pesa kupitia makampuni mbalimbali kama Puma ambayo kabla  ya hapo alikuwa akivalishwa na Adidas.

Mbali ya makampuni hayo Suarez pia ni balozi wa  Beats, Beats Abitab, Antel, Cablevision, Garnier, Pepsi, na Samsung ambazo zote kwa pamoja zinampa zaidi ya Pauni 3 milioni kwa mwaka.


MSAADA KWA JAMII

Amewahi kununua zaidi ya vifungashio 1000 vya chakula kwa ajili ya kusaidia watoto wasiojiweza huko Uruguay na mbali ya hiyo amekuwa akicheza mechi mbalimbali za kirafiki zenye lengo la kukusanya pesa kwa ajili ya kusaidia watu mbalimbali wasiojiweza.

MJENGO

Wakati anajiunga na Inter Miami alinunua mjengo unaokadiriwa kufikia Dola 11 milioni huko Florida Marekani lakini mbali ya mjengo huo anamiliki nyumba nyingine huko Hispania maeneo ya Castelldefels, Catalonia, ambayo aliinunua kwa Dola 3.6 milioni mwaka 2018.


NDINGA

Range Rover Sport-Pauni 67,000

Audi SQ7- Pauni 87,000

BMW X5, Pauni- 70,000

Audi RS6 Avant-Pauni 115,000

Cadillac Escalade-Pauni 90,000

Hyundai Tucson N-Line-Pauni -32,000

BMW iX, Pauni-69,000


MAISHA NA BATA

Yupo kwenye ndoa na  Sofía Balbi ambaye ni mchumba wake wa utotoni, wawili hawa walioana mwaka 2009 na hadi sasa wamefanikiwa kupata watoto watatu na wapili ni Benjamin Suarez ambaye anaonekana kufuata nyayo za baba yake na kwa sasa anacheza timu za vijana za Inter Miami ambapo yupo pamoja na mtoto wa Messi. Mtoto wake mkubwa zaidi ni wakike.