Atalanta yaiduwaza Liverpool nyumbani
Muktasari:
- Liverpool imekumbana na kipigo chao cha kwanza ndani ya dakika 90 za mchezo, wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani Anfield kwa mara ya kwanza tangu 2018 katika mashindano yote.
LIVERPOOL, ENGLAND. KLABU ya Atalanta ya Italia imeisapraizi Liverpool kwa kuishushia kipigo cha mabao 2-0 ndani ya dakika nne kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na kuweka hai matumaini yao ya kutinga hatua ya mtoano ya 16 Bora.
Katika mchezo wa kwanza ambao ulichezwa Italia, Atalanta wakiwa nyumbani walichezea kichapo cha mabao 5-0.
Liverpool ilijikuta ikikumbana na wakati mgumu kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Anfield na kushindwa kupiga hata shuti moja lililolenga lango la Atalanta.
Mabao ya Josip Ilicic na Robin Gosens kipindi cha pili ambayo yalifungwa dakika ya 60 na 64 yalitosha kwa Atalanta inayonolewa na Gian Piero Gasperini kuvuna pointi tatu muhimu wakiwa ugenini.
Katika mchezo huo, kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp alionekana akifanya mabadiliko kwa wachezaji wanne ambao ni Salah, Wijnaldum, Origi na Tsimikas huku wakiingia Firmino, Fabinho, Jota na Robertson lakini mabadiliko hayo yajakuzaa matunda .
Pamoja na kipigo hicho, Liverpool wataendelea kuongoza msimamo wa kundi lao D wakiwa na pointi 9 huku wakifuatiwa na Ajax pamoja na Atalanta wenye pointi saba kila mmoja ili kujihakikishia kutinga hatua ya mtoano wanatakiwa kufanya vizuri katika mchezo wao ujao.
Liverpool itacheza ugenini dhidi ya Ajax kabla ya kukabiliana na Midtjylland ambao wanaburuza mkia kwenye kundi lao wakiwa hawana pointi hata moja.
MATOKEO KAMILI
B. Monchengladbach 4 - 0 Shakhtar Donetsk
Olympiacos Piraeus 0 - 1 Manchester City
Ajax 3 - 1 Midtjylland
Atl. Madrid 0 - 0 Lokomotiv Moscow
Bayern Munich 3 - 1 Salzburg
Inter 0 - 2 Real Madrid
Liverpool 0 - 2 Atalanta
Marseille 0 - 2 FC Porto