Kipchoge akataa kustaafu riadha, kuja kivingine
Muktasari:
- Baada ya miaka 22 ya rekodi za dunia, na utendaji wa kihistoria ikiwemo marathon yake ya chini ya saa mbili ya kihistoria mnamo 2019, Kipchoge sasa anatafuta urithi unaozidi michezo ya riadha.
Bingwa wa mara mbili wa mbio za marathon za Olimpiki, Eliud Kipchoge mwenye umri wa miaka 40, amejiweka miongoni mwa wanariadha bora zaidi katika historia ya mchezo wa riadha duniani huku akiwa amekuja na jambo jipya.
Kipchoge, amejiingiza kwenye changamoto mpya ya kukimbia marathon katika kila bara ndani ya miaka miwili ijayo.
Mafanikio yake makubwa duniani katika mashindano ya marathon kutoka London na Berlin hadi Tokyo na Chicago pamoja na medali za dhahabu za Olimpiki mfululizo, yamefanya kuwa alama ya dunia kwa nidhamu, umakini na unyenyekevu. Hata hivyo, kama anavyosisitiza, mbio zake bado hazijakoma.
Baada ya kuibuka mshindi katika mashindano ya New York City Marathon, ambapo alikuwa mwanariadha wa kwanza kushiriki katika Abbott World Marathon Majors zote saba, Kipchoge ametangaza kipindi kingine cha safari yake ya kipekee ‘Eliud Kipchoge World Tour’.
“Njia pekee ya kuhudumia binadamu duniani ni kukimbia katika mabara yote saba ukihubiri injili ya kukimbia,” amesema Kipchoge.
“Hii si kustaafu, bali ni mpito nafasi ya kukimbia kwa lengo na kuhudumia binadamu.”
Mpango mpya wa Kipchoge ni kama falsafa kadri ilivyo kimwili. Anakusudia kutumia lugha ya ulimwengu ya kukimbia kuhamasisha amani, elimu, na uelewa wa mazingira, akihimiza watu kote kutoka nje, kusogea, na kuungana na dunia na nafsi zao.
“Lengo ni kuhamasisha watu kukimbia kwa ajili ya maisha yao, akili zao, nchi zao, kwa amani, kwa uzuri wa dunia hii, kwa elimu na kwa mazingira,” amefafanua.
Safari yake itampeleka mbali zaidi ya mitaa ya Berlin au London. Kutoka katika majangwa ya Afrika hadi kwenye barafu la Antarctica, kila hatua ya Kipchoge itakuwa alama ya uvumilivu kwa ajili ya kitu kikubwa kuliko ushindi na umoja wa roho ya binadamu.
“Kila mtu anataka kukimbia haraka, umri sio kizuizi. Ningeweza kustaafu, lakini bado najikakamua kushindana na vijana,” amesema.
Baada ya miaka 22 ya rekodi za dunia, na utendaji wa kihistoria ikiwemo marathon yake ya chini ya saa mbili ya kihistoria mnamo 2019, Kipchoge sasa anatafuta urithi unaozidi michezo ya riadha.