Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Jeshi la McCarthy likijiandaa kuikabili Equatorial Guinea, Senegal

Muktasari:

  • Opondo na Otiende wamepata mwaliko wao wa kwanza kwenye timu ya wakubwa baada ya kupandishwa kutoka timu ya vijana ya chini ya miaka 20 ya Kenya, Rising Stars.

Kocha wa timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, Benni McCarthy amewaita kipa Brian Opondo na beki Kevin Otiende kwenye kikosi kitakachocheza mechi za kirafiki za kimataifa dhidi ya Equatorial Guinea na Senegal.

Opondo na Otiende wamepata mwaliko wao wa kwanza kwenye timu ya wakubwa baada ya kupandishwa kutoka timu ya vijana ya chini ya miaka 20 ya Kenya, Rising Stars.

Kikosi kilichoitwa kwa mechi hizo mbili pia kinajumuisha makipa Bryne Omondi na Brian Bwire. Opondo alikuwa kwenye kikosi cha Kenya kwa michuano ya CHAN 2024, lakini hakupata nafasi ya kucheza.

McCarthy pia amewaita mabeki Kevin Otiende (Nairobi United), Bryton Onyona (Gor Mahia), na mshambuliaji Sharriff Musa (Gor Mahia) kwenye timu hiyo.

Kenya itacheza mechi hizo mbili za kirafiki mjini Antalya, Uturuki, wakati wa mapumziko ya kimataifa ya FIFA kati ya Novemba 10 na 18, 2025.

Mechi hizi mbili zimechukua nafasi ya zile zilizokuwa zimepangwa awali dhidi ya Madagascar na Comoros.

Kenya itaanza kwa kucheza dhidi ya Equatorial Guinea, Novemba 14, 2025 kwenye Uwanja wa Emir Complex mjini Antalya kuanzia saa 12 jioni kwa saa za Kenya, ikifuatiwa na mechi dhidi ya Senegal siku nne baadaye katika Uwanja wa Mardan. Timu itaingia kambini kesho Novemba 9, 2025 na kuondoka kuelekea Uturuki Jumatano Novemba 12, 2025.

Kocha McCarthy pia amewaita mabeki Sylvester Owino, Alphonce Omija, Michael Kibwage, Ronney Onyango, Kevin Otiende, na Baron Ochieng.

Viungo ni Alpha Onyango, Duke Abuya, Timothy Ouma, na Marvin Nabwire.

Washambuliaji waliomo kwenye kikosi ni Austine Odhiambo, William Lenkupae, Job Ochieng, Boniface Muchiri, Aldrine Kibet, Ovellah Ochieng, Jonah Ayunga, Ryan Ogam, Lawrence Okoth, na Sharif Musa.

Sharif na Ovellah wanarejea baada ya kukosekana kwa muda mrefu. Kibet, anayekipiga katika klabu ya Celta Vigo nchini Hispania, ameitwa kwa mara ya kwanza kwenye timu ya wakubwa baada ya kupandishwa kutoka timu ya vijana chini ya miaka 20.

Equatorial Guinea na Senegal zitazitumia mechi hizi kujiandaa kwa michuano ya AFCON 2025, itakayofanyika kuanzia Desemba 21, 2025 hadi Januari 18, 2026 nchini Morocco.

Senegal, chini ya kocha Pape Thiaw, itacheza pia mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil jijini London, Novemba 15, 2025 kabla ya kuvaana na Kenya.

Kikosi cha Senegal kinajumuisha nyota kama Edouard Mendy, Sadio Mane, Nicolas Jackson na Kalidou Koulibaly.

Equatorial Guinea ipo Kundi E la AFCON 2025 pamoja na Algeria, Burkina Faso, na Sudan, wakati Senegal ipo Kundi D na DR Congo, Benin, na Botswana.

Kenya haikufanikiwa kufuzu kwa michuano hiyo, baada ya kumaliza nafasi ya tatu katika Kundi J ikiwa na alama sita, nyuma ya Cameroon na Zimbabwe ambazo zimefuzu.

Sasa Kenya inalenga maandalizi ya AFCON 2027, ambayo itakuwa mwenyeji kwa pamoja na Uganda na Tanzania.