Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga yaanza mchakato mrithi wa Pedro, yarudi kwa Mtunisia

YANGA Pict


YANGA imeanza msako wa haraka wa kutafuta kocha mpya baada ya kuachana na Mreno, Pedro Concalves, aliyeondolewa Mei 6, 2026, saa chache tangu kumalizika kwa mechi ya Ligi Bara dhidi ya KMC.


Yanga imeachana na Pedro aliyemaliza mechi hiyo kwa ushindi mwembamba wa bao 1-0 na aliyeiongoza timu hiyo kwenye jumla ya mechi 35 za mashindano yote msimu huu tangu alipoanza Oktoba 28, 2025, akichukua nafasi ya Romain Folz.


Saa chache baada ya kuondolewa kwa Pedro, mabosi wa Yanga tena wale wa juu wakaanza kuzunguka kutafuta kocha mpya haraka na walianzia kwa Khalil Ben Youssef raia wa Tunisia kwenye hesabu za kutafuta bosi mpya wa ufundi.

YANG 01

Ben Youssef sio jina geni Yanga kwani aliwahi kufanya kazi klabuni hapo akiwa kocha msaidizi wa Nasreddine Nabi wakati akiwafundisha mabingwa hao.

Ben Youssef hakukaa sana Yanga kwani alikuja miezi michache wakati Yanga ikiwa kwenye mechi za Kombe la Shirikisho Afrika kuanzia hatua ya robo fainali msimu ambao Yanga ilikwenda kucheza fainali 2023 dhidi ya USM Alger ya Algeria, iliyokuwa bingwa.

“Tumeshaanza mazungumzo, tumeanza na yule Khalil (Ben Youssef) nadhani unamkumbuka ni kocha mzuri sana, tunaona ni bora tutafute kocha wa kisasa kijana ambaye anajua mazingira ya soka la Tanzania,” amesema bosi huyo wa juu ndani ya Yanga.

YANG 02

Mpaka sasa Ben Youssef yupo pale Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini akiwa kama kocha mkuu sambamba na Mrundi Cedric Kaze ambao walichukua nafasi hiyo baada ya timu hiyo kuachana na Nabi aliyekuwa bosi wa wawili hao.

Kocha huyo aliyezaliwa miaka 37 iliyopita, ameiongoza Kaizer kucheza mechi 10 za Kombe la Shirikisho Afrika, kati ya hizo, akishinda tano, akipoteza tatu na kutoa sare mbili na hatua ya makundi timu hiyo ilimaliza na pointi 10 ikishika nafasi ya tatu nyuma ya Al Masry nafasi ya pili na Zamalek ambayo itacheza fainali.

Kwenye ligi, Ben Youssef ameiongoza Kaizer kwenye mechi 20, kati ya hizo akishinda tisa, akipoteza nne na kutoa sare saba, timu hiyo ikiwa nafasi ya tatu na jumla ya 48 baada ya kucheza mechi 27, Orlando Pirates ikiwa nafasi ya pili na pointi 62 wakati Mamelodi Sundowns ikiongoza na pointi zao 65.

YANG 03

Katika dili hilo la Ben Youssef, linaweza kumshuhudia Mtunisia huyo akirudi na Kaze wawili hao wakirudi kwa mara nyingine endapo pande hizo mbili zitaendelea vizuri kwenye mazungumzo hayo yanayoendelea.

Kaze endapo atarejea Yanga itakuwa mara ya tatu na awali alikuja akitokea Canada lakini hakudumu, akisitishiwa safari hiyo njiani kuisha baadaye kurudi tena akiwa msaidizi wa Nabi, wakienda tena kukutana Afrika Kusini.

Ben Youssef kama akimalizana na Yanga hatakutana na wakati mgumu kutokana na mfumo wake anaopenda kuutumia wa 4-2-3-1 sio mgeni kwa wachezaji wa timu hiyo ukiwa umetumiwa na makocha mbalimbali wakiwemo Nabi, Miguel Gamondi na hata Miloud Hamdi.

Hata hivyo, wakati mchakato huo wa kuunda benchi jipa la ufundi la Yanga, klabu hiyo imetangaza kwamba hivi sasa kikosi hicho kitakuwa chini ya Abdihamid Moalin na Patrick Mabedi hadi mwisho wa msimu.