Taa zazima uwanjani Kaitaba mechi Kagera Sugar vs Geita Gold yaahirishwa

Mchezo wa Ligi Kuu kati ya Kagera Sugar dhidi ya Geita Gold FC umeahiriishwa timu zote zikiwa suluhu 0-0, ni kutokana na tatizo la umeme ndani ya Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, ukiwa umechezwa kwa dakika 39 tu.
Kwa mujibu wa Katibu wa Chama cha soka mkoani Kagera, Ally Amin Abdul kinachosubiriwa sasa ni maelekezo ya siku na muda ambao mchezo utachezwa kwa dakika zilizosalia.
Dakika zilizosalia kwa mchezo huo kumalizika ni dakika 51